-
Wamarekani wahoji: Je, Huckabee anawakilisha maslahi ya Washington au Tel Aviv?
Feb 23, 2026 03:14Kauli na matamshi ya balozi wa Marekani huko Israel, Mike Huckabee, yamesababisha hasira kubwa baada ya kusema kwamba utawala ghasibu wa Israel una haki ya kupanua eneo lake kwa kupora eneo kubwa la Mashariki ya Kati la nchi kadhaa za Kiarabu na Kiislamu, kwa mujibu wa tafsiri maarufu za Torati ndani ya harakati za Kikristo yenye msimamo mkali nchini Marekani.
-
Türk: Akili Mnemba izingatie ujumuishaji, uwajibikaji na viwango vya kimataifa
Feb 22, 2026 12:15Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki za Binadamu, Volker Türk, ameonya kuwa bila kuweka mifumo madhubuti ya udhibiti kwa haraka, akili mnemba (AI) inaweza kuongeza pengo la usawa, kuimarisha upendeleo na kusababisha madhara halisi katika jamii.
-
Pakistan: Suala la kuitambua rasmi Israel halipo kabisa katika ajenga zetu
Feb 22, 2026 06:47Waziri wa Ulinzi wa Pakistan amesisitiza kwamba, suala la kuutambua rasmi utawala wa Kizayuni wa Israel si jambo ambalo lipo katika ajenga za nchi hiyo.
-
Mjibizo hasi wa maoni ya umma wa Marekani kwa sera za kupenda vita za Trump
Feb 22, 2026 06:30Maoni ya umma nchini Marekani katika mwaka huu wa 2026, yanapinga vikali chokochoko yoyote mpya ya kijeshi dhidi ya Iran. Fikra za walio wengi nchini Marekani zina mtazamo hasi kuhusiana na sera za kupenda vita za Rais mtata Donald Trump.
-
Kwa nini Amnesty International imelaani operesheni za kijeshi za Marekani huko Karibiani na Pasifiki?
Feb 22, 2026 02:29Shirika la Amnest International limelaani mashambulizi ya Marekani katika eneo la Karibiani na huko Pasifiki.
-
Uhispania: Ilikuwa ni 'makosa' Kamishna wa EU kuhudhuria mkutano wa 'Bodi ya Amani' ya Trump
Feb 21, 2026 11:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Uhispania Jose Manuel Albares amesema, ilikuwa ni "makosa" kwa Kamishna wa Umoja wa Ulaya kuhudhuria mkutano wa uzinduzi wa 'Bodi ya Amani' ya Rais wa Marekani Donald Trump mjini Washington.
-
Wabunge wa Marekani wanataka kupiga kura kuzuia mamlaka ya Trump ya kushambulia Iran
Feb 21, 2026 07:35Wabunge wa Marekani huenda wakapiga kura mapema wiki ijayo juu ya muswada unaolenga kumzuia Rais Donald Trump kuanzisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Iran bila idhini ya wazi ya Bunge la Marekani.
-
Mwandishi wa NY Times: Netanyahu anamtumia vibaya Trump kwa ajili ya vita na Iran
Feb 21, 2026 03:05Mwandishi maarufu wa gazeti la Marekani la New York Times, Thomas Friedman, ameonya kwamba waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu anamhadaa Rais wa Marekani, Donald Trump, na makundi ya jamii ya Wayahudi wa Marekani ili kuendeleza malengo yake ya kisiasa yenye utata, ikiwa ni pamoja na kuongezeka mvutano na Iran.
-
Kupinga Wabunge wa Marekani sera za Trump za kupiga ngoma ya vita dhidi ya Iran
Feb 21, 2026 02:19Wimbi la upinzani limeibuka miongoni mwa Wabunge wa Marekani dhidi ya sera za Rais Donald Trump zinazochochea vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais wa zamani wa Korea Kusini afungwa maisha jela
Feb 20, 2026 03:26Mahakama ya Korea Kusini jana Alkhamisi ilimhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo, Yoon Suk Yeol kifungo cha maisha jela kwa kutangaza sheria ya kijeshi mnamo Desemba 2024, na kumtia hatiani mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 65 kwa kuongoza uasi na kuhujumu katiba.