-
Siasa za kupinga uhamiaji huko Los Angeles zaibua mvutano kati ya serikali ya shirikisho na za majimbo?
Jun 09, 2025 10:13Hitilafu kuhusu siasa za kupinga uhamiaji na jinsi ya kukabiliana na waandamanaji huko Los Angeles zimeibua mvutano mkali kati ya serikali ya shirikisho ya Marekani na serikali ya Jimbo la California.
-
Polisi Marekani watumia risasi kuwatawanya waandamanaji Los Angeles
Jun 09, 2025 06:58Maafisa wa usalama nchini Marekani wametumia gesi ya kutoa machozi na risasi za plastiki katika mji wa Los Angeles siku ya Jumapili, kufuatia hatua ya Rais Donald Trump kupeleka jeshi linalojulikana kama Gadi ya Kitaifa kwa ajili ya kukandamiza maandamano yaliyozuka kupinga dhulma dhidi wahamiaji.
-
Mgombea urais Colombia apigwa risasi kwenye mkutano wa kampeni za uchaguzi
Jun 08, 2025 12:32Mgombea urais wa Colombia amepigwa risasi tatu wakati akiwa katika hafla ya kampeni katika mji mkuu, Bogota. Miguel Uribe Turbay, (39), alishambuliwa alipokuwa akihutubia umati mdogo katika bustani siku ya Jumamosi.
-
Kwa nini Marekani imewawekea vikwazo majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai?
Jun 08, 2025 06:45Marekani mnamo Alhamisi, Juni 5, iliwawekea vikwazo majaji wanne wa kike wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai kwa kushughulikia kesi zinazohusiana na Israel na hatua za Marekani nchini Afghanistan. Vikwazo hivyo, ambavyo mara nyingi huwekewa maafisa kutoka nchi zinazopinga Marekani, sasa vimewalenga maafisa wa mahakama ya kimataifa.
-
Ufaransa yasisitiza kuhusu azma ya kutambua taifa la Palestina
Jun 07, 2025 12:58Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noël Barrot, amesema kuwa Paris bado imejizatiti kutambua rasmi taifa la Palestina katika mkutano wa Umoja wa Mataifa unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.
-
UN yakemea vikali vikwazo vya Marekani dhidi ya majaji wa ICC
Jun 07, 2025 12:37Volker Türk Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu, amelaani uamuzi wa hivi karibuni wa serikali ya Marekani wa kuweka vikwazo dhidi ya majaji wanne wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), akisema kuwa hatua hiyo inahatarisha misingi ya utawala bora na usimamizi huru wa haki.
-
UN: Tumesikitishwa mno na vikwazo vya US dhidi ya majaji wa ICC
Jun 07, 2025 06:59Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Turk amesema "amesikitishwa sana" na vikwazo vya serikali ya Marekani dhidi ya majaji wanne wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC).
-
Wafanyakazi wa bandari Ufaransa, Italia wazuia kupelekwa silaha Israel
Jun 07, 2025 06:58Wafanyakazi wa bandari za Ufaransa na Italia wameendelea kufanya mgomo wao na kukataa kupakia shehena za silaha na zana za kijeshi zinazopelekwa Israel, wakisema kuwa hawatahusika katika "mauaji ya halaiki" yanayoendelea Gaza.
-
Chuo cha Trinity Ireland chakata uhusiano na Isreal kulalamikia mauaji ya Gaza
Jun 07, 2025 02:32Chuo Kikuu cha Trinity cha Iralend kimekata uhusiano wake na utawala haramu wa Israel kama hatua ya kulalamikia jinai zinazofanywa na utawala huo dhidi ya wakazi wa Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Uswahiba wa Trump na Elon Musk wazidi kuharibika baada ya kurushiana matusi
Jun 07, 2025 02:29Uswahiba huba wa Rais wa Marekani Donald Trump na mfanyabiashara tajiri zaidi duniani Elon Musk sasa unaonekana kufikia ukingoni baada ya wawili hao kurushiana cheche za maneno makali na hata matusi kwenye mitandao ya kijamii.