-
Wabunge wa Uingereza watoa wito wa kufukuzwa Marekani katika mashindano ya Kombe la Dunia 2026
Jan 15, 2026 07:46Wabunge wapatao ishirini wa Bunge la Uingereza wamelitaka Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kuiondoa Marekani katika fainali za Kombe la Dunia 2026, licha ya kuwa mwenyeji mkuu, kwa sababu ya mienendo ya Rais wa Marekani, Donald Trump, na ukiukaji wake wa mamlaka ya nchi huru.
-
Haki za binadamu za Kimarekani; Risasi ndani, madai ya haki za binadamu nje ya nchi
Jan 15, 2026 05:11Kufuatia kifo cha raia wa Marekani aliyepigwa risasi na maafisa wa uhamiaji, maandamano yamekuwa yakiendelea katika majimbo mengi ya Marekani.
-
Wakazi wa Greenland: Hatutaki kuwa Wamarekani
Jan 14, 2026 06:26Akthari ya wakazi wa eneo la Greenland wamesema wanahofia kwamba Rais wa Marekani, Donald Trump atatekeleza kivitendo tishio lake la kulitwaa eneo hilo, wakisisitiza kuwa katu hawataki kuwa raia wa Marekani.
-
Je, tishio la ushuru la Trump ni ishara ya nguvu au kukiri kushindwa?
Jan 14, 2026 02:38Katika matamshi yake mapya ya vitisho, Rais wa Marekani amezililenga nchi zinazofanya biashara na Iran.
-
China: Tunapinga vitisho vya ushuru vilivyotolewa na Trump dhidi ya washirika wa kibiashara wa Iran
Jan 13, 2026 10:30Serikali ya China imetangaza kuwa inapinga vitisho vya ushuru vilivyotolewa na Rais wa Marekani dhidi ya nchi zinazoshirikiana kibiashara na Iran.
-
Seneta Warner: Serikali ya Trump inachangia kueneza chuki dhidi ya Uislamu na Waarabu ndani ya Marekani
Jan 13, 2026 10:30Seneta wa Marekani Mark Warner amesema, nchi hiyo inakabiliwa na ongezeko la ubaguzi wa kidini na misimamo ya kufurutu mpaka inayochochewa na chuki, akiishutumu serikali ya Trump kwa kuchangia kuongezeka kwa hisia za uenezaji hofu na chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na hisia za kupiga vita Waarabu.
-
Wataalamu: Uingiliaji wa kigeni wanaoutaka Wairani ni wa kusaidia kuondolewa vikwazo vya Marekani
Jan 13, 2026 10:29Maandamano yaliyoikumba Iran yamechochewa na mbinyo mkubwa wa kiuchumi; na kutokana na Wairani kuona jinai zilizofanywa na Israel na kile ambacho Marekani imekifanya nchini Venezuela, madai hasa ya wananchi hao si kutaka ufanyike uingiliaji wa kijeshi wa madola wageni dhidi ya nchi yao. Hayo yameelezwa na wataalamu kadhaa wa kikanda.
-
Medvedev 'amdhihaki' Trump: Usipoharakisha, Greenland itapiga kura ya kujiunga na Russia
Jan 13, 2026 10:29Naibu Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la Russia Dmitry Medvedev amesema, Wagreenland wanaweza kupiga kura ya maoni ya kujiunga na Russia ikiwa Rais wa Marekani Donald Trump hatachukua hatua haraka kukinyakua kisiwa hicho cha ncha ya kaskazini, Aktiki.
-
ICJ yaanza kusikiliza kesi ya mauaji ya kimbari ya Waislamu wa Rohingya dhidi ya Myanmar
Jan 13, 2026 03:42Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) jana ilianza kusikiliza kesi kubwa dhidi ya Myanmar kwa kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Waislamu wa Rohingya, kabila la walio wachache kutoka Jimbo la Rakhine nchini Myanmar.
-
Russia yaangusha ndege ya kivita ya Kimarekani aina ya F‑16 ya jeshi la Ukraine
Jan 12, 2026 10:14Mifumo ya ulinzi wa anga ya Russia imefanikiwa kuiangusha ndege ya kivita ya F‑16 Eagle iliyotengenezwa Marekani, ambayo ilikuwa ikitumiwa na jeshi la anga la Ukraine.