-
58% ya Wamarekani wanaunga mkono kulitambua taifa la Palestina
Aug 21, 2025 08:13Asilimia 58 ya Wamarekani wanaunga mkono hatua ya nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa zinazolitambua rasmi taifa la Palestina. Hii ni kwa mujibu wa uchunguzi mpya ya maoni ulioandamana na matumaini kuwa Israel na Hamas zinaweza kufikia makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Wafuasi wa Trump wakasirishwa na kutoroka kwa afisa wa Israel anayetuhumiwa kwa uhalifu wa kingono
Aug 21, 2025 08:12Vuguvugu la MAGA (Make America Great Again) linaushinikiza utawala wa Trump kueleza ni kwa nini afisa wa serikali ya Israel aliyekamatwa katika operesheni ya siri dhidi ya unyanyasaji wa kingono kwa watoto huko Nevada aliruhusiwa kuondoka Marekani baada ya kuachiliwa kwa dhamana.
-
ICC: Vikwazo vya US ni hujuma dhidi ya mamilioni ya wahanga wa jinai
Aug 21, 2025 02:13Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetumia maneno makali kuilaani Marekani, kwa hatua yake ya hivi karibuni ya kuwawekea vikwazo majaji wa mahakama hiyo, kutokana na juhudi zao za kuwafungulia mashitaka maafisa Marekani na Israel wanaotuhumiwa kuhusika na uhalifu wa kivita na aina nyingine za ukatili.
-
Makocha wa Soka wa Italia wataka Israel itimuliwe kwenye Mashindano ya FIFA na UEFA
Aug 20, 2025 23:31Kabla ya mchezo muhimu wa kufuzu Kombe la Dunia kati ya Italia na Israel, Chama cha Makocha wa Italia (AIAC), kinachojulikana pia kama Assoallenatori, kimeomba rasmi mashirika ya soka ya kimataifa kuiondoa Israel katika mashindano ya soka ya kimataifa.
-
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu kuongezeka mauaji ya wahudumu wa misaada ya kibinadamu
Aug 20, 2025 08:59Umoja wa Mataifa umeonya kuhusu kuongezeka mauaji ya wahudumu wa misaada ya kibinadamu.
-
Waziri mkuu wa Australia apuuza shutuma za Netanyahu
Aug 20, 2025 08:45Waziri mkuu wa Australia Anthony Albanese leo amepuuza shutuma za Benjamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala ghasibu wa Israel dhidi ya uamuzi wa nchi hiiyo wa kulitambua taifa la Palestina, na kusema anawaheshimu viongozi wa nchi nyingine.
-
Makumi ya watu wafariki dunia katika ajali ya barabarani magharibi mwa Afghanistan
Aug 20, 2025 03:01Msemaji wa Serikali ya Jimbo la Herat magharibi mwa Afghanistan amesema kuwa ajali mbaya ya barabarani katika jimbo hilo imeua watu 71, wakiwemo watoto 17.
-
Kiongozi wa Korea Kaskazini aagiza silaha za nyuklia ziwekwe tayari kukabiliana na Marekani
Aug 19, 2025 23:22Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, ameitaka nchi yake kuongeza haraka uwezo wake wa nyuklia kutokana na kile alichokitaja kama “uchochezi wazi wa vita” kupitia mazoezi ya kijeshi ya pamoja ya Marekani na Korea Kusini.
-
‘Haikubaliki’: Australia yaikosoa Israel kwa kubatilisha visa za maafisa wake
Aug 19, 2025 23:07Australia imeikosoa Israel kwa kubatilisha visa za mabalozi wake waliokuwa na mamlaka kwa Mamlaka ya Wapalestina, hatua iliyotambuliwa kama ulipizaji kisasi baada ya Canberra kukataa kumkaribisha mwanasiasa wa mrengo wa kulia wa Israel.
-
Mkutano wa Washington kwa ajili ya amani nchini Ukraine; misukumo na changamoto
Aug 19, 2025 22:48Mkutano wa viongozi wa Ulaya na Marekani kuhusu Ukraine ulifanyika mjini Washington siku ya Jumatatu.