-
Ubelgiji kupiga marufuku simu za mkononi maskulini kuanzia mwaka wa masomo wa 2025-2026
Aug 19, 2025 02:42Matumizi ya simu za mkononi na vifaa vingine vya kielektroniki yatapigwa marufuku nchini kote Ubelgiji katika skuli za msingi na sekondari kuanzia mwaka wa masomo wa 2025-2026, isipokuwa vitakapolazimu kutumika kwa sababu za kimasomo, kiafya, au za dharura. Hayo yameripotiwa na vyombo vya habari vya ndani ya nchi hiyo.
-
Israel yazuiwa kushiriki maonyesho ya biashara ya Italia
Aug 18, 2025 23:36Utawala wa kizayuni wa Israel umepigwa marufuku kushiriki katika maonyesho ya biashaya Italia.
-
Waliokufa kwa maafa ya mafuriko Pakistan wapindukia 600
Aug 18, 2025 23:23Idadi ya watu waliopoteza maisha kufuatia janga la mafuriko nchini Pakistan imeongezeka na kupindukia 600.
-
Kwa nini viongozi wa Ulaya wanaandamana na Zelensky katika safari yake ya Washington?
Aug 18, 2025 23:15Baadhi ya viongozi wa Ulaya, wameamua kuandamana na Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine katika safari yake ya kwenda Washington katika hatua ya kidiplomasia ya kuunga mkono misimamo ya Ukraine katika mazungumzo yake na Rais Donald Trump wa Marekani dhidi ya mashinikizo ya nchi hiyo ya kumtaka akubali haraka makubaliano ya amani.
-
Makanisa ya Uholanzi yatangaza kuitambua Palestina
Aug 18, 2025 07:26Makanisa 73 ya Kiprotestanti nchini Uholanzi yametoa taarifa ya kuitaka serikali ya nchi hiyo kulitambua taifa la Palestina na kuacha kupeleka shehena ya silaha kwa utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Uruguay yafunga ofisi yake Quds kuonyesha mshikamano na Gaza
Aug 17, 2025 23:24Serikali ya Uruguay imeamua kusitisha makubaliano ya ushirikiano yaliyotiwa saini mwezi Disemba mwaka jana 2024 kati ya Wakala wa Kitaifa wa Utafiti na Ubunifu wa Uruguay na chuo kikuu cha Israel huko Quds (Jerusalem) inayokaliwa kwa mabavu, sanjari na kufunga Ofisi yake ya Ubunifu mjini Jerusalem ili kuonyesha mshikamano na Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Maelfu waandamana mjini New York kupinga sera ya njaa huko Gaza
Aug 17, 2025 07:54Maelfu ya wananchi wa Marekani wameshiriki maandamano huko mjini New York kutaka kukomeshwa utumiaji wa njaa kwa makusudi dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza, sambamba na kuchukuliwa hatua za haraka za kimataifa za kukomesha mauaji ya halaiki katika eneo hilo.
-
Trump anataka mazungumzo ya pande tatu baina yake na Putin na Zelensky yafanyike Agosti 22
Aug 17, 2025 03:49Rais wa Marekani Donald Trump amekusudia kufanya mkutano wa pande tatu na viongozi wenzake wa Russia na Ukraine siku ya Ijumaa ya tarehe 22 Agosti. Hayo ni kwa mujibu wa tovuti ya habari ya Axios.
-
Ni yapi matokeo ya mkutano wenye utata wa Trump na Putin?
Aug 16, 2025 07:57Hatimaye, baada ya kusubiri kwa muda mrefu na uvumi kuhusu mkutano kati ya Marais Donald Trump wa Marekani na Vladimir Putin wa Russia kuhusu vita vya Ukraine, mkutano huo hatimaye ulifanyika Ijumaa, Agosti 15 huko Alaska.
-
Idadi ya waliofariki dunia kwa mafuriko Pakistan yapindukia 300
Aug 16, 2025 07:23Idadi ya watu waliopoteza maisha yao kufuatia janga la mafuriko nchini Pakistan imeongezeka na kufikia 337.