-
Duru ya nne ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja baina ya Iran na Marekani kuanza kesho
May 10, 2025 07:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Oman, Badr Al-Busaidi, ambaye anakaimu nafasi ya mpatanishi kati ya Iran na Marekani katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja, ametangaza kuwa duru ya nne ya mazungumzo hayo itafanyika mjini Muscat kesho Jumapili.
-
Araghchi kufanya safari Saudi Arabia na Qatar kwa shughuli za kidiplomasia
May 09, 2025 10:54Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anatazamiwa kuzuru Saudi Arabia na Qatar Jumamosi ya kesho ikiwa ni sehemuu ya juhudi mpya za kuimarisha uhusiano na majirani wa eneo hili.
-
Araqchi: Iran iko tayari kupatanisha kati ya India na Pakistan
Apr 26, 2025 07:05Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi ametangaza kwamba Tehran iko tayari "kufanya juhudi za kuzidisha maelewano kati ya India na Pakistan katika kipindi hiki kigumu.
-
Iran: Utawala wa Kizayuni ndio kizuizi pekee kwa Asia Magharibi kuwa eneo lisilo na silaha za nyuklia
Apr 20, 2025 05:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Abbas Araghchi amesema utawala wa Kizayuni wa Israel ndio kizuizi pekee kwa Asia Magharibi kuwa eneo lisilo na silaha za nyuklia, akionya kwamba utawala huo unaokalia ardhi kwa mabavu unachochea chuki dhidi ya Iran huku wenyewe ukiendeleza mauaji ya kimbari katika eneo hili.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Israel haina uthubutu wa kutushambulia
Apr 20, 2025 02:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: "si Israel pekee ambayo haina uthubutu wa kutushambulia, lakini hata Marekani pia haikubali kubahatisha kujiingiza kwenye chokochoko hatari kama hiyo."
-
Araqchi: Uhusiano wa Iran na Russia ni imara na wa kimkakati
Apr 19, 2025 02:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi ameutaja uhusiano wa Iran na Russia kuwa ni imara mno na kwamba Moscow ni mshirika mkuu na wa kistratijia wa Iran.
-
Iran yazionya nchi jirani: Jihadharini na ufitinishaji na ufarakanishaji wa Marekani
Mar 25, 2025 12:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amezungumzia tuhuma zilizotolewa na viongozi wa Marekani kuhusiana na kuiwekea mashinikizo Iran na akasema: "inavyotarajiwa, nchi jirani na marafiki zitajihadhari na ufitinishaji na ufarakanishaji unaofanywa na Marekani".
-
Iran: Marekani haina haki ya kutupangia tufuate siasa gani
Mar 16, 2025 06:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma ujumbe akisisitiza kuwa, Marekani haina haki ya kutupangia tufuate siasa gani za kigeni.
-
Iran: Machafuko nchini Syria ni kwa manufaa ya Israel
Mar 09, 2025 06:47Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, machafuko na ukosefu wa utulivu nchini Syria ni kwa manufaa ya utawala wa Kizayuni na kwamba magenge ya kigaidi na yenye misimamo mikali yanatumia vibaya fursa hiyo kwa manufaa yao binafsi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Ulimwengu wa Kiislamu uchukue msimamo thabiti kuiunga mkono Palestina
Feb 17, 2025 07:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekumbusha kuhusu uungaji mkono ulioonyeshwa na nchi za Kiarabu na Kiislamu kwa hatua ya maana iliyochukuliwa na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu OIC ya kukabiliana na mpango wa pamoja wa Marekani na utawala wa Kizayuni unaolenga kuifuta Palestina, na akabainisha kwamba: "Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuiunga mkono Palestina kwa msimamo thabiti."