Jan 15, 2017 14:32
Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, Tehran imekuwa ikikabiliwa na ukiukwaji wa ahadi, kigugumizi, siasa za ucheleweshaji mambo na chuki za Marekani na baadhi ya nchi katika utekelezwaji wa makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA).