-
Vyombo vya habari Marekani: Trump anataka kumteua rais wa FIFA kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
Jul 22, 2026 10:19Rais wa Marekani, Donald Trump, anataka kumteua Rais wa FIFA, Gianni Infantino katika nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
-
Baqaei: Marekani imeonyesha tena sera yake ya uharibifu kwa kushambulia miundombinu ya Iran
Jul 20, 2026 11:20Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Esmaeil Baqaei amesema kuwa Marekani imeonyesha kwa mara nyingine tena sera yake ya uharibifu baada ya kufanya mashambulizi dhidi ya miundombinu ya Iran.
-
Malalamiko rasmi dhidi ya Infantino wa FIFA kuhusu uhusiano Wake na Trump
Jul 11, 2026 04:32Shirika moja la kutetea haki za binadamu na usimamizi wa michezo limetangaza mpango wake wa kuwasilisha malalamiko dhidi ya Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino, kwa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC). Shirika hilo linamtuhumu Infantino kwa kukiuka mara kwa mara sheria za kutofungamana na upande wowote katika masuala ya kisiasa, kupitia uungaji mkono wake wa wazi na uhusiano wa karibu na Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Trump amwambia Netanyahu katika malumbano makali ya simu: "Wayahudi wote wamekuchoka"
Jun 26, 2026 11:16Televisheni ya CNN ya Marekani imefichua malumbano makali ya simu baina ya Rais wa Marekani na Waziri Mkuu wa Israel ambapo Donald Trump amemkemea Benjamin Netanyahu, akimwambia: "Wayahudi wote wamekuchoka," huku Marekani ikizidisha mashinikizo kwa ajili ya kufikia makubaliano kuhusu Ukanda wa Gaza.
-
Kiongozi Muadhamu apongeza juhudi za maafisa wa Iran, asema Trump alitamani sana kufikia makubaliano
Jun 19, 2026 04:02Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei amesema maafisa wa Iran wamefanya juhudi kubwa kwa nia njema kufikia makubaliano ya maelewano na Marekani, huku rais wa Marekani akitumia njia mbalimbali za mashinikizo kutokana na kukata tamaa.
-
Baada ya Trump kusherekea bethidei yake ya 80, sasa umri na afya ndio kiini cha mjadala wa kisiasa wa Marekani
Jun 16, 2026 02:53Ripoti ya Newsweek inaonyesha kwamba kutimiza umri wa miaka 80 Rais wa Marekani Donald Trump kumerejesha mjadala wa umri na afya ya rais katika mstari wa mbele wa malumbano ya kisiasa nchini Marekani, baada ya yeye mwenyewe kufanya umri na utimamu wa akili wa mtangulizi wake, Joe Biden kuwa moja ya mada kuu za kampeni yake ya uchaguzi.
-
Washington Post: Trump anasherehekea kurudi katika hali ya kabla ya vita na Iran
Jun 15, 2026 10:09Gazeti la Washington Post, katika ripoti yake kuhusu hati ya makubaliano kati ya Iran na Marekani, limekejeli hatua ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kusherehekea kurejea Washington kwenye hali ya kabla ya Februari 28, hatua ambayo baadhi ya wataalamu wanaamini ni kurudi nyuma kwa maana halisi ya neno hilo mkabala wa Iran.
-
Bunge la Marekani lapitisha hatua ya kupunguza mamlaka ya vita ya Trump dhidi ya Iran
Jun 04, 2026 03:32Baraza la Wawakilishi la Marekani limeidhinisha azimio linalolenga kupunguza mamlaka ya vita ya Rais Donald Trump kuhusiana na Iran, ikiwa ni ishara ya changamoto kubwa kwa jinsi utawala wa Trump unavyoshughulikia uchokozi wake dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Shirikisho la Soka la Norway laiomba FIFA kuchunguza tuzo ya amani ya Trump
Jun 03, 2026 04:07Shirikisho la Soka la Norway (NFF) lilisema jana Jumanne kwamba limeiomba kamati ya maadili ya FIFA kuchunguza tuzo ya amani iliyotolewa na baraza linalosimamia soka duniani kwa Rais wa Marekani, Donald Trump.
-
Israel yafuta mpango wa kushambulia Beirut baada ya onyo kali la Iran
Jun 02, 2026 09:12Utawala wa Israel umeachana na mpango wake wa kufanya mashambulizi makali ya ya kijeshi dhidi ya mji mkuu wa Lebanon, Beirut. Haya yameelezwa siku ya Jumatatu na Rais wa Marekani, Donald Trump, kufuatia onyo kali kutoka kwa Iran kwamba haitavumilia wimbi jipya la uvamizi dhidi ya Beirut, hatua ambayo ingekiuka makubaliano ya kusitisha vita kati ya Iran na Marekani.