-
Kaburi la pamoja kuchimbwa ndani ya hospitali Gaza ili kuzika maiti 100 za waliouliwa na mashambulio ya Israel
Nov 11, 2023 09:24Wizara ya Afya ya Palestina katikia Ukanda wa Gaza imetangaza leo kuwa kaburi la pamoja litachimbwa ndani ya hospitali ya Al-Shifa ili kuzika maiti 100 zilizokuwa zimetawanyika hospitalini humo, za watu waliouawa shahidi kwa mashambulio ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Khatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Nchi za Kiarabu zinapaswa kukata uhusiano na utawala wa Kizayuni
Nov 10, 2023 08:07Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesisitiza ulazima wa serikali za nchi za Kiarabu kujibu ipasavyo matukio yanayojiri Ukanda wa Gaza na kusema: Jambo dogo kabisa linalotarajiwa kutoka kwa serikali za nchi za Kiarabu ni kukata uhusiano na utawala ghasibu wa Israel.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mashinikizo ya kisiasa yazidishwe dhidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni
Nov 06, 2023 10:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza udharura wa kuongezeka mashinikizo ya kisiasa ya Ulimwengu wa Kiislamu dhidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ili kusimamisha mauaji yanayofanywa dhidi ya watu wa Gaza na kusema: Iraq, ikiwa nchi muhimu katika eneo la Magharibi mwa Asia, inaweza kuwa na nafasi maalumu katika uwanja huu na kuanzisha mstari mpya katika ulimwengu wa Waarabu na wa Kiislamu.
-
Mpira wa kusimamisha au kupanua wigo wa vita Ghaza uko katika uwanja wa Netanyahu na jeshi la Kizayuni
Nov 05, 2023 03:22Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa inakaribia kufika mwezi mmoja tangu itekelezwe huku jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel likiendelea kuwaua watu wa Ghaza na kujaribu kufidia kushindwa kwao katika vita vya nchi kavu kwa kuwaua raia kwa umati.
-
Misimamo inayogongana ya White House na Biden kuhusu kusitishwa mapigano huko Ghaza
Nov 02, 2023 23:57Ikiwa zimepita takribani wiki 4 tangu kuanza operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa na mashambulizi ya jinai ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa maelfu ya Wapalestina hususan watoto na wanawake, Marekani ambayo ni muungaji mkono mkuu na mshirika wa kistratijia wa utawala wa Kizayuni, bado inataka kuendelezwa mauaji ya umwagaji damu huko Ghaza.
-
Kwa mara ya kwanza rais wa Marekani ataka kuwepo 'usitishaji' katika vita vya Israel dhidi ya Gaza
Nov 02, 2023 09:41Rais Joe Biden wa Marekani, kwa mara ya kwanza ametoa sauti ya kuunga mkono "usitishaji" mapigano kwa sababu za kibinadamu katika vita vya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza wakati Washington inatilia mkazo kuwaondoa Wamarekani wote waliokwama katika eneo hilo la Palestina lililowekewa mzingiro.
-
Kuendelea siasa za undumakuwili za Erdogan kuhusu uungaji mkono kwa watu wa Gaza
Nov 02, 2023 08:18Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki anaendeleza siasa zake za undumakuwili katika kuunga mkono watu wa Ghaza, huku ndege za kivita za kistratijia za Marekani zikiwa zimeegeshwa katika kituo cha kijeshi cha Incirlik kusini mwa Uturuki.
-
"Okoa watoto wa Gaza", Wamarekani wakatiza kikao cha Kongresi cha kumsaili Blinken na Austin
Nov 01, 2023 04:45Waandamanaji jana Jumanne walikatiza kikao cha kuwahoji mawaziri wa Mambo ya Nje na Ulinzi wa Marekani katika Bunge la Kongresi kilichoitishwa kwa ajiili ya kijadili suala la kuongeza uungaji mkono na misaada kwa Israel na Ukraine. Waandamanaji hao walioingia ndani ya Kongresi walitoa nara wakitaka "kuokolewa watoto wa Gaza" na "kusitishwa mapigano mara moja" katika eneo hilo la Palestina.
-
Al-Azhar: Adui Mzayuni ni mbwa mwitu mkali aliyepatwa na kichaa cha kuua
Nov 01, 2023 04:40Taasisi ya kidini ya Al-Azhar nchini Misri imetangaza kuwa: “Adui Mzayuni amegeuka na kuwa mbwa mwitu mkali na mwenye kiu ya kuua watoto, wanawake na watu wasio na hatia, na kufurahia kula nyama zao na kunywa damu zao bila ya kizuizi chochote.
-
Waziri wa Afya wa Iran akosoa kimya cha WHO kwa jinai za Israel katika Ukanda wa Gaza
Oct 31, 2023 06:42Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa kimya cha Shirika la Afya Duniani (WHO) kwa jinai zinazofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.