May 02, 2023 07:34
Martin Griffiths, mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kabla ya kuelekea nchini Sudan kwamba hali ya kibinadamu nchini humo ni mbaya sana kiasi kwamba imefikia kwenye hatua ya kusambaratika kabisa. Amesema, utatuzi wa mgogoro wa Sudan hauwezi kupatikana kutokana na kuendelea vita hivyo.