-
Ujumbe wa HAMAS wa Sikukuu ya Idul Fitr
Mar 30, 2025 07:41Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetoa ujumbe wa Sikukuu ya Idul Fitr kwa kuyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kuongeza juhudi na uungaji mkono kwa Wapalestina ili kukomesha jinai za Israel na kuondolewa mzingiro kwenye Ukanda wa Ghaza.
-
Radiamali ya Hamas kufuatia kuuliwa shahidi "Abdel-Latif al-Qanoua" katika hujuma ya Israel
Mar 27, 2025 22:59Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imeashiria katika taarifa yake kuhusu kuuawa shahidi Abdel-Latif al-Qanoua Msemaji wa harakati hiyo katika shambulio la utawala wa Kizayuni na kutangaza kuwa: "Kuwalenga kwa masambulizi viongozi wa harakati ya Hamas na wasemaji wake kamwe hakuwezi kuvunja irada yetu.
-
Kukiri jamii ya ujasusi ya Marekani kwamba Hamas haijashindwa huko Gaza
Mar 27, 2025 22:57Ripoti kuhusu vitisho ambayo hutolewa kila mwaka na jamii ya masuala ya ujasusi ya Marekani imekiri kwamba kundi la muqawama wa Palestina la Hamas huko Gaza halijashindwa bado na kwamba linaendelea kudumisha nguvu, wapiganaji na miundombinu yake.
-
Hamas yataka walimwengu wajitokeze kwa wingi kuiunga mkono Palestina Siku ya Quds
Mar 27, 2025 07:39Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imetoa mwito wa kuhamasishwa walimwengu kujitokeza kwa wingi katika siku za Ijumaa, Jumamosi na Jumapili ili kuonyesha mshikamano na Gaza na al-Quds wakati huu ambapo Israel, kwa uungaji mkono wa Marekani, inaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina Gaza, mkabala wa kimya cha dunia.
-
Siku ya Quds, Jihadul Islami yasisitiza: Muqawama bado una nguvu
Mar 26, 2025 22:53Ziad Al-Nakhala, Katibu Mkuu wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina ametoa hotuba kwa mnasaba wa maandalizi ya Siku ya Kimataifa ya Quds akiwapongeza mashahidi wa Operesheni Kimbunga cha al Aqsa na kusema: "Malengo yetu ni ya hali ya juu na adhama yetu ni kubwa. Wazayuni wauaji na washirika wao hawawezi kuvunja irada yetu, na tunazidi kuwa na nguvu. Muqawama wetu unaweka historia isiyosahaulika leo hii."
-
HAMAS: Netanyahu anaongopa akidai vita vitawarejesha mateka wote wakiwa hai
Mar 26, 2025 07:41Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imemshutumu Waziri Mkuu wa Israel, Benjami Netanyahu kwa "kudanganya familia za [mateka], anapodai kuwa chaguo la kijeshi lina uwezo wa kuwarejesha (mateka wote) wakiwa hai."
-
HAMAS: Uvunjeni mzingiro, komesheni mauaji na hitimisheni kuteswa Wapalestina kwa njaa
Mar 25, 2025 08:53Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa taarifa ya kulaani "mauaji ya kutisha" yanayoendelea kufanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel na kuitolea mwito Jamii ya Kimataifa ichukue hatua za kuudhibiti utawala huo dhalimu.
-
HAMAS haitokwama kwa kuuliwa shahidi viongozi wake
Mar 25, 2025 03:16Kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amesema kuwa, عtawala wa Kizayuni unajidanganya unapodhani kwamba utaweza kuiangamiza Hamas kwa kuwaua shahidi makamanda wake.
-
Hamas: Mauaji ya Wapalestina akiwemo Mbunge yataimarisha Muqawama
Mar 23, 2025 07:29Jeshi la Israel limefanya mashambulizi mapya ya kutisha ya anga katika Ukanda wa Gaza na kuua shahidi watu wasiopungua 40, akiwemo Salah al-Bardawil, Mbunge wa Palestina na Mjumbe wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas.
-
HAMAS yaisihi dunia: Msiiache Ghaza 'inayovuja damu' iyakabili 'mauaji ya halaiki' peke yake
Mar 20, 2025 23:56Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa ombi la kuchukuliwa hatua za haraka kukomesha "uangamizaji kizazi wa kimpangilio unaofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel na kuwatesa kwa njaa makusudi Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza", jinai ambazo imesema, "zinafanywa kwa usaidizi wa kuaibisha wa kimaitaifa usioweza kuhalalishwa".