-
Abdollahian: Lugha ya vitisho dhidi ya Iran haitaambulia chochote
Aug 13, 2022 22:31Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani inapaswa kufahamu kuwa, kutumia lugha ya vitisho dhidi ya taifa la Iran hakutakuwa na manufaa yoyote kwa Washington.
-
Marandi: Matukio kuhusu Bolton na Salman Rushdie yanatia shaka
Aug 13, 2022 06:41Mshauri wa timu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika mazungumzo ya uondoaji vikwazo huko Vienna ameshangazwa na sadfa ya matukio mawili ya hivi karibuni huko Marekani, na kuashiria kuwa yumkini matukio hayo yanafungamana na mazungumzo ya kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran: Marekani haiwezi kuficha jinai zake kwa kuibua madai bandia
Aug 12, 2022 21:02Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kitendo cha Marekani cha kuibua tuhuma na madai yasiyo na msingi wala mashiko yoyote hakiwezi kuficha wala kuhalalisha jinai za serikali ya Washington.
-
China: Vikwazo vya US vimeisababishia Iran hasara ya dola bilioni 200
Aug 12, 2022 21:00China imesema vikwazo haramu na vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran vimelisababishia taifa hili la Kiislamu hasara ya mabilioni ya dola.
-
Jeshi la Majini la Iran lazima shambulio la maharamia Bahari Nyekundu
Aug 11, 2022 03:24Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuwa makomandoo wa jeshi hilo wamezima hujuma ya maharamia dhidi ya meli ya kibiashara ya Iran katika Bahari Nyekundu.
-
Iran yajitenga na madai ya kijuba ya kutaka kumuua Bolton
Aug 11, 2022 02:54Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imepinga madai ya kiwendawazimu na yasiyo na msingi yaliyotolewa na serikali ya Washington ikidai kuwa raia mmoja wa nchi hii alikula njama ya kumuua John Bolton, mshauri wa zamani wa Usalama wa Kitaifa wa Ikulu ya White House ya Marekani.
-
Wairani waandamana kulaani ukatili wa Israel dhidi ya wakazi wa Gaza
Aug 10, 2022 06:54Wananchi wa Iran jana Jumanne walifanya maandamano katika mji mkuu Tehran kulaani jinai za utawala wa Kizayuni za kuwaua shahidi wanawake na watoto wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Marekani yatiwa kiwewe na hatua ya Iran kurusha satalaiti anga za mbali
Aug 10, 2022 06:51Marekani imeghadhabishwa na hatua ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ya kurusha satalaiti katika anga za mbali kwa mafanikio, kwa kutumia roketi la Russia.
-
Satalaiti ya Khayyam; hatua muhimu katika harakati ya Iran ya kuzitumia anga za mbali
Aug 09, 2022 21:00Waziri wa Habari na Mawasiliano na Teknolojia wa Iran Issa Zarepour ametangaza kuwa satalaiti ya Kiirani ya Khayyam jana Jumanne ilipaa kuelekea anga za mbali umbali wa kilomita 500 kutoka ardhini.
-
Abdollahian awapongeza wanamuqwama kwa kukabiliana na wanajeshi wa Kizayuni
Aug 09, 2022 20:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwa mara nyingine tena wanajihadi za harakati za muqawama wa Palestina wameweza kusimama kidete mkabala wa nguvu kubwa za kijeshi za utawala wa Kizayuni, na hatimaye wakawalazimisha maadui kusalimu amri na kuafiki kusitisha vita.