-
Iran yashambulia kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Oman, Qatar na Bahrain, yafunga Lango Bahari la Hormuz
Jul 12, 2026 04:20Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo asubuhi vimetekeleza operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Qatar, Oman na Bahrain, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi endelevu ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Onyo kali la Majeshi ya Iran: Uchokozi wa Marekani katika Lango la Hormuz utajibiwa haraka
Jul 03, 2026 03:45Kamandi Kuu ya Majeshi ya Iran, maarufu kama Kamandi ya Khatam al-Anbiya, imetoa onyo kali kuwa, uingiliaji wowote wa kijeshi wa Marekani katika Lango Bahari la Hormuz utajibiwa kwa kasi na maamuzi madhubuti na vikosi vya ulinzi vya Iran, huku ikisisitiza kuwa njia hiyo muhimu ya bahari iko chini ya mamlaka kamili ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Iran: Waliohusika na mauaji ya wanafunzi wa shule ya Minab wachukuliwe hatua
Jun 26, 2026 04:21Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amelaani "uhalifu mbaya" uliofanywa na Marekani katika shule ya Msingi ya Shajareh Tayyebeh ya Minab nchini Iran wakati wa mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kislamu, na kutoa wito kwa wahusika wote, wapangaji na viongozi kuwajibishwa kikamilifu, akisisitiza kwamba: "Kumbukumbu ya watoto wa Minab inahitaji haki, uwajibikaji na utekelezaji, si kukaa kimya."
-
Qalibaf: Mkataba wa Islamabad ni tangazo la kufeli kwa Marekani
Jun 24, 2026 11:00Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Mkataba wa Maelewano (MoU) wa kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa matokeo ya shinikizo au kulazimishwa, bali ni zao la ustahimilivu na nguvu ya taifa shupavu la Iran.
-
'Kujisalimisha kikamilifu' kwa Iran: Wabunge wa Marekani washambulia MoU ya Trump na Iran
Jun 18, 2026 12:33Wakielezea hati ya maelewano kati ya Iran na Marekani kuwa ni "kujisalimisha kikamilifu" kwa Iran, wakosoaji wa Donald Trump katika Bunge la marekanii wamesema utawala wake umesalimu amri kwa Jamhuri ya Kiislamu baada ya vita vya gharama kubwa na visivyo na maana ambavyo vilishindwa kufikia malengo yaliyotajwa na Washington.
-
Viongozi wa dunia wakaribisha makubaliano ya kumaliza vita vya Marekani dhidi ya Iran
Jun 15, 2026 04:28Viongozi mbalimbali duniani wamekaribisha hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani, ambayo inahitimisha mara moja vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na Israel dhidi ya Iran, kuondoa mzingiro wa baharini, na kufungua tena Lango Bahari la Hormuz kwa usafiri wa kimataifa.
-
Majeshi ya Iran yashambulia ngome za kijeshi za Marekani kujibu uchokozi
Jun 11, 2026 11:42Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Bei za mafuta zapanda duniani kutokana na ukiukaji wa usitishaji vita wa Marekani dhidi ya Iran
Jun 11, 2026 11:38Bei za mafuta ghafi ya petroli zilipanda Alhamisi duniani kufuatia kurejea kwa mashambulizi ya kijeshi baada ya uchokozi wa Marekani na ukiukaji wake wa makubaliano ya kusitisha mapigano na Iran. Mvutano huo umeongeza wasiwasi kuhusu usambazaji wa nishati duniani pamoja na kuendelea kwa usumbufu wa usafirishaji kupitia Mlango wa Hormuz.
-
Gazeti la NYT: Shambulio la Marekani dhidi ya miundombinu ya maji nchini Iran ni uhalifu wa kivita
Jun 11, 2026 11:09Gazeti mashuhuri la The New York Times limesema kuwa mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya miundombinu ya maji kusini mwa Iran yanaweza kuhesabika kama uhalifu wa kivita, kwani kulenga miundombinu ya kiraia ni kinyume kabisa na sheria za kimataifa.
-
WFP: Vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinasukuma mamilioni kukumbwa na njaa Afrika
Jun 06, 2026 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limeonya kuwa vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran vinawasukuma mamilioni ya watu duniani kuingia katika hali ya njaa huku bara Afrika likionekana kuathirika zaidi.