-
Reuters: Duru ya pili ya mazungumzo ya Iran na Marekani itafanyika Jumanne, Geneva
Feb 14, 2026 09:56Shirika la habari la Reuters limenukuu chanzo kimoja na kutangaza kuwa ujumbe wa Marekani unaojumuisha Steve Witkoff na Jared Kushner, utakutana na maafisa wa Iran mjini Geneva, Uswisi siku ya Jumanne wiki hii.
-
Iran yasisitiza kuwa itavishambulia vituo vya kijeshi vya Marekani, si ardhi za nchi jirani
Feb 08, 2026 06:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, iwapo Marekani itaishambulia Iran, vituo vya kijeshi vya nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi navyo vitashambuliwa.
-
Waziri wa Fedha wa US akiri hadharani: Tulisababisha uhaba wa dola ndani ya Iran ili kuchochea machafuko
Feb 08, 2026 02:30Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Kenneth Homer Bessent amekiri kuwa, Washington ilisababisha uhaba wa sarafu ya dola ya nchi hiyo ndani ya Iran, hatua ambayo ilisababisha kushuka kwa kasi kwa thamani ya sarafu ya Iran ya riali na kuibua mashinikizo ya kiuchumi yaliyochochea machafuko ya Desemba mwaka jana.
-
Mtaalamu wa kijeshi: Utitiri wa droni za Iran ni 'tishio halisi' kwa vyombo vya majini vya Marekani
Jan 28, 2026 10:32Mtaalamu wa kijeshi wa ndege zisizo na rubani ameonya kuwa, utitiri wa ndege zisizo na rubani za Iran ni "tishio halisi" kwa vyombo vya jeshi la wanamaji la Marekani vyenye thamani kubwa, wakati huu ambapo Washington inaripotiwa kuwa inaendelea kujizatiti kijeshi katika eneo la Asia Magharibi.
-
Yemen yatoa onyo la kuishambulia manowari ya Marekani ikikiuka mzingiro wa Bahari Nyekundu
Jan 28, 2026 10:20Harakati ya Ansarullah ya Yemen, leo imetoa indhari kwa kukumbusha shambulio lake la huko ililofanya kwa mafanikio dhidi ya meli ya mafuta ya Uingereza ya "Marlin Luanda" katika Ghuba ya Aden kufuatia ukiukaji wa mzingiro wa majini uliowekwa na harakati hiyo dhidi ya Israel,
-
Uhalali wa kisheria wa Iran kujihami dhidi ya vitisho vya Marekani
Jan 27, 2026 12:30Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lazima lieleze ukiukwaji uliofanywa na Marekani kwa uwazi na kwa majina yao halisi.
-
Kwa nini njama zote za Marekani dhidi ya Iran daima zinafeli?
Jan 16, 2026 02:10Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kwamba, watu wa Iran wataendelea kusimama imara kulinda na kutetea nchi yao, akisisitiza kuwa, njama yoyote ya Marekani dhidi ya Iran itashindwa tu kama zilivyoshindwa njama zao zote za huko nyuma.
-
Kamanda: Baada ya kushindwa vita vya Juni, US na Israel zinaendesha 'vita laini' kuvuruga utulivu Iran
Jan 05, 2026 03:17Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel zinaendesha "vita laini" ili kuvuruga uthabiti na utulivu nchini likiwa ni jaribio la kufidia kushindwa kwao katika vita vya siku 12 vya mwezi Juni zilivyoanzisha dhidi ya Iran.
-
Iran yajibu vitisho vya Trump, yaapa kwamba 'jibu kali' litatolewa kwa uchokozi wowote
Dec 30, 2025 03:26Admirali Ali Shamkhani, Mshauri mwandamizi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amelaani vikali vitisho vipya vilivyotolewa na Marekani vya kuishambulia kijeshi Jamhuri ya Kiislamu, akiapa kuwa jibu kali litatolewa endapo utafanywa uchokozi wowote ule.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Mzozo uliopo kati ya Iran na Marekani ni wa dhati halisi na wa migongano ya maslahi
Nov 03, 2025 13:25Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, mzozo uliopo kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani ni wa "dhati halisi" na wala hautokani na kauli mbiu; na chimbuko lake liko kwenye mgongano wa kimsingi wa maslahi; na akaeleza bayana kwamba, suala la ushirikiano na Marekani linaweza kuja kufikiriwa siku za usoni na si sasa hivi wala katika muda wa karibu,