-
Araghchi: Iran na US zinapiga hatua 'karibu zaidi kufikia mwafaka' katika baadhi ya masuala
Feb 27, 2026 03:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema duru ya karibuni ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana na Marekani iliyofanyika jana mjini Geneva, Uswisi ilikuwa moja ya mazungumzo bora, mazito zaidi, na marefu zaidi kuwahi kufanyika hadi sasa, na kwamba Tehran na Washington zimepiga hatua za "karibu zaidi kufikia mwafaka" katika baadhi ya masuala.
-
Iran yapinga “uongo mkubwa” wa Marekani kuhusu kadhia ya nyuklia
Feb 26, 2026 06:13Iran imepinga vikali madai mapya ya Marekani kuhusu shughuli zake za nyuklia na makombora, pamoja na takwimu za waliouawa katika machafuko ya hivi karibuni, ikiyataja kuwa ni “msururu wa uongo mkubwa” huku ikikosoa kampeni iliyoratibiwa ya upotoshaji wa taarifa dhidi yake.
-
Iran yamuonya Trump asichukue maamuzi yanayotegemea taarifa za uongo
Feb 26, 2026 03:51Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amemuonya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya kufanya maamuzi yanayotegemea taarifa zisizo sahihi, akisisitiza kuwa Iran haijawahi kutafuta, haitafuti, wala haitawahi kutafuta silaha za nyuklia.
-
Araghchi asisitizia fursa ya kufikia mwafaka na US, kulindwa mamlaka ya nchi kwa gharama yoyote
Feb 25, 2026 07:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema Iran na Marekani zina "fursa ya kihistoria" iliyopo mbele ya macho ya kufikia "makubaliano ambayo hayajawahi kushuhudiwa," huku akionya kwamba Jamhuri ya Kiislamu italinda uhuru na mamlaka yake ya kujitawala kwa gharama yoyote endapo kutakuwa na uvamizi mpya wa kijeshi wa Marekani.
-
Kutokubali Iran kusalimu amri mbele ya Marekani
Feb 24, 2026 02:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akijibu mshangao wa Rais wa Marekani kuhusu sababu za Iran kutokubali kusalimu amri, aliandika kwa uwazi: “Hatusalimu amri kwa sababu sisi ni Wairani.”
-
Iran, US zakamilisha duru ya pili ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana ya nyuklia, Geneva
Feb 17, 2026 13:39Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, duru ya pili ya mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya ana kwa ana kati ya Iran na Marekani imemalizika mjini Geneva, Uswisi.
-
Reuters: Duru ya pili ya mazungumzo ya Iran na Marekani itafanyika Jumanne, Geneva
Feb 14, 2026 09:56Shirika la habari la Reuters limenukuu chanzo kimoja na kutangaza kuwa ujumbe wa Marekani unaojumuisha Steve Witkoff na Jared Kushner, utakutana na maafisa wa Iran mjini Geneva, Uswisi siku ya Jumanne wiki hii.
-
Iran yasisitiza kuwa itavishambulia vituo vya kijeshi vya Marekani, si ardhi za nchi jirani
Feb 08, 2026 06:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, iwapo Marekani itaishambulia Iran, vituo vya kijeshi vya nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi navyo vitashambuliwa.
-
Waziri wa Fedha wa US akiri hadharani: Tulisababisha uhaba wa dola ndani ya Iran ili kuchochea machafuko
Feb 08, 2026 02:30Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Kenneth Homer Bessent amekiri kuwa, Washington ilisababisha uhaba wa sarafu ya dola ya nchi hiyo ndani ya Iran, hatua ambayo ilisababisha kushuka kwa kasi kwa thamani ya sarafu ya Iran ya riali na kuibua mashinikizo ya kiuchumi yaliyochochea machafuko ya Desemba mwaka jana.
-
Mtaalamu wa kijeshi: Utitiri wa droni za Iran ni 'tishio halisi' kwa vyombo vya majini vya Marekani
Jan 28, 2026 10:32Mtaalamu wa kijeshi wa ndege zisizo na rubani ameonya kuwa, utitiri wa ndege zisizo na rubani za Iran ni "tishio halisi" kwa vyombo vya jeshi la wanamaji la Marekani vyenye thamani kubwa, wakati huu ambapo Washington inaripotiwa kuwa inaendelea kujizatiti kijeshi katika eneo la Asia Magharibi.