-
Baghaei: Iran haizishambulii nchi jirani, inavilenga vituo na maslahi ya Marekani tu katika eneo
Mar 05, 2026 05:24Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, Esmail Baghaei amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haizishambulii nchi jirani, bali inavilenga vituo vya kijeshi na vya maslahi ya Marekani vilivyoko katika eneo hili.
-
Nara za “Mauti kwa Marekani” zatanda kwenye anga ya barabara za Rome na Vienna
Mar 03, 2026 12:42Mamia ya wanachama wa asasi zinazopinga vita, wanaharakati wa haki za binadamu na wapinzani wa uchokozi wa kijeshi wa Marekani na utawala wa kizayuni dhidi ya Iran wameandamana katika mitaa na barabara kuu za miji ya Rome, Italia na Vienna, Austria huku wakipiga nara na kaulimbiu za “Mauti kwa Marekani”.
-
Araghchi: Iran na US zinapiga hatua 'karibu zaidi kufikia mwafaka' katika baadhi ya masuala
Feb 27, 2026 00:01Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema duru ya karibuni ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana na Marekani iliyofanyika jana mjini Geneva, Uswisi ilikuwa moja ya mazungumzo bora, mazito zaidi, na marefu zaidi kuwahi kufanyika hadi sasa, na kwamba Tehran na Washington zimepiga hatua za "karibu zaidi kufikia mwafaka" katika baadhi ya masuala.
-
Iran yapinga “uongo mkubwa” wa Marekani kuhusu kadhia ya nyuklia
Feb 26, 2026 02:43Iran imepinga vikali madai mapya ya Marekani kuhusu shughuli zake za nyuklia na makombora, pamoja na takwimu za waliouawa katika machafuko ya hivi karibuni, ikiyataja kuwa ni “msururu wa uongo mkubwa” huku ikikosoa kampeni iliyoratibiwa ya upotoshaji wa taarifa dhidi yake.
-
Iran yamuonya Trump asichukue maamuzi yanayotegemea taarifa za uongo
Feb 26, 2026 00:21Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amemuonya Rais wa Marekani Donald Trump dhidi ya kufanya maamuzi yanayotegemea taarifa zisizo sahihi, akisisitiza kuwa Iran haijawahi kutafuta, haitafuti, wala haitawahi kutafuta silaha za nyuklia.
-
Araghchi asisitizia fursa ya kufikia mwafaka na US, kulindwa mamlaka ya nchi kwa gharama yoyote
Feb 25, 2026 03:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema Iran na Marekani zina "fursa ya kihistoria" iliyopo mbele ya macho ya kufikia "makubaliano ambayo hayajawahi kushuhudiwa," huku akionya kwamba Jamhuri ya Kiislamu italinda uhuru na mamlaka yake ya kujitawala kwa gharama yoyote endapo kutakuwa na uvamizi mpya wa kijeshi wa Marekani.
-
Kutokubali Iran kusalimu amri mbele ya Marekani
Feb 23, 2026 22:51Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, akijibu mshangao wa Rais wa Marekani kuhusu sababu za Iran kutokubali kusalimu amri, aliandika kwa uwazi: “Hatusalimu amri kwa sababu sisi ni Wairani.”
-
Iran, US zakamilisha duru ya pili ya mazungumzo yasiyo ya ana kwa ana ya nyuklia, Geneva
Feb 17, 2026 10:09Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, duru ya pili ya mazungumzo ya nyuklia yasiyo ya ana kwa ana kati ya Iran na Marekani imemalizika mjini Geneva, Uswisi.
-
Reuters: Duru ya pili ya mazungumzo ya Iran na Marekani itafanyika Jumanne, Geneva
Feb 14, 2026 06:26Shirika la habari la Reuters limenukuu chanzo kimoja na kutangaza kuwa ujumbe wa Marekani unaojumuisha Steve Witkoff na Jared Kushner, utakutana na maafisa wa Iran mjini Geneva, Uswisi siku ya Jumanne wiki hii.
-
Iran yasisitiza kuwa itavishambulia vituo vya kijeshi vya Marekani, si ardhi za nchi jirani
Feb 08, 2026 02:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, iwapo Marekani itaishambulia Iran, vituo vya kijeshi vya nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi navyo vitashambuliwa.