-
Uwanja wa ndege wa Tripoli, Libya walengwa kwa kombora
Sep 12, 2018 03:09Duru za habari leo asubuhi zimeripoti kuwa uwanja wa ndege wa Tripoli mji mkuu wa Libya umeshambuliwa kwa kombora.
-
Hizbullah kwa mara ya kwanza imezindua aina mbalimbali za makombora yake
Aug 19, 2018 10:51Harakati ya Hizbullah ya Lebanon kwa mara ya kwanza ilipanga kuzindua leo Jumapili sehemu ya makombora yaliyotumiwa na harakati hiyo ya muqawama wa Kiislamu kwa ajili ya kuilinda nchi hiyo katika miaka ya karibuni.
-
Jinamizi la kuendelea kupigwa Saudia kwa makombora ya Wayemen
Jun 13, 2018 02:07Turki al Maliki, msemaji wa muungano vamizi wa Saudi Arabia dhidi ya Yemen ametangaza kuwa hadi sasa Wayemen wameshavurumisha makombora 149 upande wa Saudia.
-
Makombora ya Yemen yaulenga mji mkuu wa Saudia, Riyadh
May 09, 2018 21:56Wanajeshi wa Yemen wametumia makombora yaliyoundwa nchini humo kushambulia maeneo kadhaa ya kijeshi na kiuchumi ya Saudia Arabia ukiwemo mji mkuu wa nchi hiyo, Riyadh.
-
Syria: Hivi sasa tuna uwezo mkubwa wa kutungua makombora ya adui
Apr 17, 2018 09:51Mshauri wa Rais Bashar al-Assad wa Syria, Bouthaina Shaaban amesema kuwa, jeshi la Syria limethibitisha uwezo mkubwa wa makombora yake hasa baada ya kukabiliana vilivyo na shambulizi la hivi karibuni la Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya nchi hiyo.
-
Jeshi la Syria latungua makombora 9 yaliyolenga viwanja vya ndege vya kijeshi
Apr 16, 2018 23:18Jeshi la Syria mapema leo asubuhi limetungua makombora tisa ambayo yalikuwa yamelenga viwanja vya ndege vya kijeshi vya Shayrat mkoani Homs na Al Dumayr katika viunga vya mji mkuu Damascus.
-
Iran, Russia zatoa onyo kali baada ya US, UK na Ufaransa kuvurumisha makombora Syria
Apr 14, 2018 02:45Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Russia zimelaani vikali mashambulizi ya makombora ya Marekani, Uingereza na Ufaransa dhidi ya Syria huku zikitoa onyo kali juu ya matokeo mabaya ya hujuma hiyo ya kijeshi dhidi ya nchi huru.
-
Marekani yaiuzia Qatar makombora 5000 huku mgogoro na Saudia ukitokota
Apr 11, 2018 00:05Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imetangza idhini ya kuiuzia Qatar makombora 5000 yenye thamani ya dola milioni 300 huku mgogoro baina ya nchi hiyo ndogo na Saudia ukizidi kutokota.
-
Ansarullah ya Yemen yavurumisha kombora katika kambi ya Jeshi la Saudia huko Najran
Mar 31, 2018 10:43Kitengo cha Makombora cha Harakati ya Ansarullah ya Yemen kimetangaza kuwa kimevurumisha kwa mafanikio kombora la balistiki ambalo limelenga kituo cha Jeshi la Saudia katika mkoa wa Najran kusini mwa ufalme huo.
-
Ufaransa yataka kusimamishwa mpango wa makombora wa Iran
Mar 08, 2018 12:29Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema anachukua hatua kadhaa kwa lengo la kuhakikisha mpango wa makombora ya balisitiki wa Iran unasimamishwa.