Feb 05, 2016 07:11
Huku mapigano katika maeneo tofauti ya Yemen yakipamba moto, Saudi Arabia imeendelea kukwamisha juhudi za kidiplomasia za kuutatua kisiasa mgogoro huo, suala ambalo limewafanya wanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa kusema kuwa, ni jambo lililo mbali kufikiria kufanyika mazungumzo hayo katika siku za hivi karibuni.