-
Russia: Marekani imekiuka mkataba wa silaha za kibaolojia
Apr 04, 2022 21:51Naibu mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa, Dmitry Polyansky, ameuambia mkutano wa waandishi wa habari mjini New York kwamba shughuli za kijeshi za kibaolojia za Marekani nchini Ukraine zinakiuka Mkataba wa Silaha za Kibaolojia.
-
Kwa mara ya kwanza katika historia: Bunge la Pakistan latoa nara ya "Mauti kwa Marekani"
Apr 04, 2022 03:07Kwa mara ya kwanza katika historia ya Bunge la Pakistan, wabunge wa nchi hiyo wametoa nara ya "Kifo kwa Marekani" huku bunge hilo likipinga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, iliyotaka kumuondoa madarakani Imran Khan, ambaye ameyatuhumu madola ya kigeni kuwa yanaingilia demokrasia ya nchi hiyo.
-
Rais wa Iran azitaka nchi za eneo zisipuuze njama za kibeberu za US-Israel
Apr 03, 2022 22:06Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema nchi yoyote katika eneo la Asia Magharibi itayopuuza njama na malengo ya kibeberu ya Marekani na utawala wa Kizayuni, itakuwa imepuuza maslahi ya taifa lake, na itaandamwa na ghadhabu za mataifa ya Kiislamu.
-
Jahromi: Marekani inasalia kuwa adui wa kudumu wa taifa la Iran
Apr 02, 2022 08:35Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema vikwazo vipya vya Washington dhidi ya raia wa Iran vinaonyesha wazi kuwa, Marekani inasalia kuwa adui wa kudumu wa taifa hili.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China Wasisitiza Udharura wa Kukabiliana na Vikwazo Haramu
Apr 02, 2022 03:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Hossein Amir-Abdollahian na mwenzake wa China, Wang Yi wamejadili masuala ya pande mbili, kieneo na kimataifa pembezoni mwa mkutano wa tatu wa mawaziri wa mambo ya nje wa nchi jirani na Afghanistan.
-
Mashambulizi dhidi ya askari wa US yameongezeka kwa 400% tangu auawe Soleimani
Apr 01, 2022 22:05Washington imekiri kuwa, tangu Luteni Jenerali Qasem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) auawe kigaidi nchini Iraq, mashambulizi dhidi ya askari wa Marekani yameongezeka kwa asilimia 400.
-
Askofu wa zamani wa US akiri: Nilificha kufanyiwa ukatili wa kingono watoto kwa miaka 25
Mar 30, 2022 02:34Aliyekuwa Askofu wa Kanisa Katoliki katika jimbo la New York nchini Marekani amejitokeza na kukiri wazi kuwa alificha na kunyamazia kimya ufuska wa kudhalilishwa na kufanyiwa ukatili wa kingono watoto wadogo na makasisi wa kanisa hilo kwa miaka 25.
-
China yaikosoa Magharibi kwa sera za kindumakuwili kuhusu haki za binadamu
Mar 29, 2022 22:29China imezishutumu nchi za Magharibi kwa kutumia sera za kindumakuwili kwa kushughulikia kwa wakati haki za binadamu za watu wanaokimbia vita vya Russia na Ukraine na kupuuza haki za wakimbizi kutoka nchi za Mashariki ya Kati, Afrika na Amerika ya Kusini.
-
Khatibzadeh: Kufanyika mkutano wa uovu ni usaliti kwa lengo tukufu la ukombozi wa Palestina
Mar 28, 2022 22:23Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kufanyika mkutano wa uovu Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kuuelezea kuwa ni usaliti kwa lengo tukufu la ukombozi wa Palestina.
-
Abbas akosoa undumakuwili wa nchi za Magharibi kuhusu vita vya Russia na Ukraine
Mar 28, 2022 21:01Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) Mahmoud Abbas amezikemea nchi za Magharibi kwa kutumia sera za kinafiki na kindumakuwili baada ya kuchukua hatua kali dhidi ya Russia kuhusu operesheni yake ya kijeshi nchini Ukraine huku zikipuuza uhalifu unaofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina.