-
Mamia ya wahajiri wa Kiethiopia wauawa kwa kupigwa risasi na askari wa Saudia
Aug 13, 2020 22:27Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limeripoti kuwa makumi ya wahajiri wa Kiethiopia waliokimbia vita kaskazini mwa Yemen wameuawa kwa kupigwa risasi na askari wa mpakani wa Saudi Arabia.
-
Bin Salman aitwa mahakamani Washington kujibu tuhuma za kutaka kumuua al Jabri
Aug 11, 2020 01:04Mahakama ya Washington DC imemtaka mrithi wa ufalme wa Saudi Arabia, Muhammad bin Salman na wenzake 13 kufika mahakamani kujibu tuhuma za kufanya jaribio la kutaka kumuua kigaidi Saad al Jabri, mkuu wa zamani wa Idara ya Intelijensia la Saudi Arabia aliyekimbilia nchini Canada.
-
Washington Post: Saudia inaongozwa na mwanamfalme wa makundi ya mauaji
Aug 10, 2020 05:21Gazeti la Washington Post la Marekani limefanya ulinganisho baina ya mauaji yaliyofanywa na Saudi Arabia dhidi ya mwandishi habari na mkosoaji wa utawala wa kifalme wa nchi hiyo, Jamal Khashogi, na jaribio la mauaji ya kigaidi lililofanywa na watu wa karibu na mrithi wa ufalme wa nchi hiyo Muhammad bin Salman dhidi ya mkuu wa zamani wa Idara ya Intelijensia la Saudi Arabia, Saad al Jabri na kusema Saudi Arabia inaongozwa na mrithi wa ufalme anayesimamia makundi ya mauti.
-
Machafuko yatanda katika mji wa Port Sudan kutokana na hitilafu za kikabila
Aug 10, 2020 05:20Gavana wa jimbo la Bahrul Ahmar nchini Sudan amepiga marufuku watu kutembea katika baadhi ya mji wa Port Sudan ambao ni wa pili kwa ukubwa nchini Sudan kutokana na ghasia zilizotokana na hitilafu za kikabila ambazo zimesababisha mauaji ya watu kadhaa na kujeruhi makumi ya wengine.
-
Mauaji ya uhamishoni; jinai kwa mtindo wa mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia
Aug 07, 2020 23:53Saad al-Jabri, Mkuu wa zamani wa Idara ya Intelijensia ya Saudi Arabia ambaye kwa sasa anaishi uhamishoni nchini Canada amewasilisha mashtaka katika mahakama moja ya Marekani akisema kuwa, Muhammad bin Salman mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudia mwaka 2018 alituma timu ya kumuua yeye, ingawa njama za mauaji hayo zilisambaratishwa na viongozi wa Canada.
-
Makumi ya wafungwa wauawa katika shambulizi la Daesh huko Afghanistan, madazani wajeruhiwa
Aug 03, 2020 06:28Zaidi ya watu 21 wameuawa katika shambulizi lililofanywa usiku wa kuamkia leo na wapiganaji wa kundi la kigaidi la Daesh katika jela moja iliyoko katika mji wa Jalalabad nchini Afghanistan.
-
Mkosoaji wa Rais wa Sudan akimbilia Marekani baada ya Rais Kiir kuamuru auawe
Jul 24, 2020 09:18Mchumi mashuhuri na mkubwa wa Sudan Kusini amekimbilia nchini Marekani bakidai kuwa, Rais Salva Kiir alikuwa ametoa amri ya kuuliwa kwake au kutekwa nyara akiwa Nairobi nchini Kenya.
-
Al Bashir kupandishwa kizimbani leo, huwenda akahukumiwa kifo
Jul 21, 2020 03:43Rais wa zamani wa Sudan na wenzake 16 wanapandishwa kizimbani leo katika mahakama maalumu ya Khartoum kwa tuhuma za kufanya mapinduzi dhidi ya serikali iliyokuwa imechaguliwa na wananchi hapo mwaka 1989.
-
Ufaransa kufungua mashtaka dhidi ya mrithi wa mtawala wa Abu Dhabi kwa kuhusika na mateso Yemen
Jul 18, 2020 22:20Viongozi wa Ufaransa wameamua kufanya uchunguzi juu ya madai kwamba mrithi wa mtawala wa Abu Dhabi, Mohammed bin Zayed Al Nahyan amehusika katika vitendo vya mateso huko Yemen, ambako Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) pamoja na Saudi Arabia na washirika wao, wamekuwa wakipigana vita vya umwagaji damu vya miaka mingi dhidi ya taifa la Yemen.
-
Mkuu wa jeshi la Somalia anusurika kifo, raia mmoja auawa katika shambulizi la al Shabab
Jul 13, 2020 22:01Mkuu wa jeshi la Somalia amenusurika jaribio la kumuua lililofanyinwa kwa gari lilikokuwa limeshehena mabomu lililotaka kuvamia msafara wake mjini Mogadishu.