-
Jihad Islami: Kuondolewa Netanyahu madarakani ni miongoni mwa mafanikio ya operesheni ya "Panga la Quds"
Jun 04, 2021 22:01Harakati ya Jihad Islami ya Palestina imetangaza kuwa moja kati ya matunda ya opesheni ya "Panga la Quds" ni kuondolewa madarakani Waziri Mkuu wa utawala ghasibu wa Israel, Benjamin Netanyahu.
-
UN: Israel ikome kuyasaidia magenge ya Wazayuni wenye silaha dhidi ya Wapalestina
Jun 03, 2021 06:51Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya jamii za waliowachache ameitaka Israel ikome kuyasaidia magenge yenye silaha dhidi ya Wapalestina wanaoishi katika ardhi zilizokaliwa kwa mabavu mwaka 1848.
-
Serikali ya Paestina yataka kusitishwa ujenzi wa vitongoji vya walowezi unaofanywa na Israel
Jun 02, 2021 23:20Wizara ya Mambo ya Nje ya Palestina imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutekeleza majukumu yao mkabala na jinai za kila siku zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel za kujenga vitongoji vya walowezi wa Kizayuni katika ardhi za Palestina.
-
HAMAS: Mzingiro dhidi ya Ukanda wa Gaza unaelekea kuvunjika
Jun 01, 2021 03:26Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema wananchi wa Palestina wamekaribia sana kuuvunja mzingiro dhidi ya Ukanda wa Gaza uliowekwa na utawala wa Kizayuni tokea mwaka 2007.
-
Wapalestina waandamana Ghaza wakitaka kufukuzwa Mkurugenzi wa UNRWA
May 31, 2021 22:21Maelfu ya raia wa Palestina jana waliandamana katika Ukanda wa Ghaza wakitaka kufukuzwa katika eneo hilo Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi wa Palestina (UNRWA).
-
Meli ya Israel yazuiwa kutia nanga nchini Marekani kutokana na jinai za Wazayuni
May 31, 2021 02:52Vyama kadhaa vya ushirika vya Marekani vimeizuia meli ya utawala wa Kizayuni isitie nanga katika bandari moja ya Auckland nchini Marekani kutokana na jinai kubwa zilizofanywa na Israel dhidi ya watoto wa Palestina.
-
Brigedia Jenerali Qaani: Wazayuni waondoke mara moja katika ardhi za Wapalestina
May 29, 2021 08:02Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema wakati umefika kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kuondoka katika ardhi za Wapalestina unaozikalia kwa mabavu haraka iwezekanavyo.
-
Maafisa usalama wa Misri wawasili katika Ukanda wa Ghaza, Palestina
May 29, 2021 05:10Duru za habari zimetangaza kuwa ujumbe maalumu wa maafisa usalama wa Misri umewasili katika Ukanda wa Ghaza huko Palestina kwa ajili ya kufanya mazungumzo na wakuu wa makundi ya muqawama.
-
Waindonesia waandamana kulaani uungaji mkono wa US kwa Israel
May 28, 2021 08:01Wananchi wa Indonesia wamefanya maandamano nje ya ubalozi wa Marekani na ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Jakarta kulalamikia na kulaani uungaji mkono wa Marekani kwa jinai za utawala haramu wa Israel.
-
Leo Wapalestina wanafanya maandamano makubwa ya kupinga Uzayuni
May 27, 2021 22:11Vijana wa Palestina wametangaza kuwa, leo Ijumaa watafanya maandamano makubwa katika kona zote za Palestina, maandamano ambayo yatapewa jina la "Mapambazuko."