-
Miaka 74 baada ya Siku ya Nakba
May 16, 2022 06:23Miaka 74 iliyopita, utawala haramu na bandia wa Kizayuni wa Israel ulitangaza uwepo wake baada ya kufanya jinai kadhaa za kinyama dhidi ya Wapalestina.
-
Iran: Njia pekee ya kupatikana haki za Wapalestina ni serikali na wananchi wa mataifa ya Waislamu kuunga mkono Muqawama
May 14, 2022 00:16Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa kuwadia kumbukumbu ya Siku ya Nakba na kusisitiza kuwa, wananchi na viongozi wa mataifa ya Waislamu inapasa watambue kuwa njia pekee ya kupatikana haki za watu wa Palestina ni kuwepo umoja na mshikamano wa Kiislamu na uungaji mkono wa serikali na wananchi wa mataifa ya Waislamu pamoja na watetezi wa ukombozi duniani kwa Muqawama wa kukabiliana na maghasibu na watumiaji mabavu.
-
Kiongozi Muadhamu: Inatarajiwa ulimwengu wa Kiarabu utaingia medani ya kisiasa kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni
May 12, 2022 23:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema dhulma ya miongo kadhaa ya utawala khabithi wa Kizayuni dhidi ya watu wa Palestina ni ukweli mchungu wa historia na pigo kwa ulimwengu wa Kiislamu na Kiarabu na kuongeza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inataraji kwamba ulimwengu wa Kiarabu utaingia wazi wazi katika medani ya kisiasa kukabiliana na jinai hizo.
-
Jordan: Masjidul-Aqswa ni mali ya Waislamu, Israel yatakiwa kutoitahini subira ya Waislamu bilioni 2
May 09, 2022 03:00Kamati ya Palestina katika Bunge la Jordan imesisitiza kuwa, Waislamu wana mamlaka mutlaki kwa msikiti mtakatifu wa al-Aqswa ulioko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Brigedi za al-Qassam: Tutatoa jibu kali kwa Israel endapo itathubutu kuua viongozi wa muqawama
May 08, 2022 00:09Msemaji wa Brigedi za al Qassam ambazo ni tawi la kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameuonya utawala haramu wa Israel na hatua yoyote ya kijinga ya kuwaua viongozi wa muqawama.
-
Hatibu wa Swala ya Ijumaa Tehran: Wazayuni sasa wanazingirwa na kambi ya muqawama
May 06, 2022 08:02Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Tehran amesema, adui Mzayuni amezingirwa na wanamapambano wa Kiislamu.
-
HAMAS: Wazayuni wana kiwewe cha kutokea tena vita vya "Upanga wa Quds"
May 06, 2022 03:11Kiongozi mmoja wa ngazi zajuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palesitna HAMAS amesema kuwa, Wazayuni bado wana kiwewe cha uzoefu mchungu wa operesheni ya "Upanga wa Quds" na hawataki kabisa kupata uzoefu mchungu mwingine kama huo.
-
"Wananchi wa Palestina wako tayari kuuhami kikamilifu Msikiti wa al Aqsa"
May 05, 2022 22:05Sekretarieti ya Mkutano wa Kimataifa wa Kuunga mkono Intifadha ya Palestina katika Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) imetoa taarifa na kulaani uvamizi wa Wazayuni katika Msikiti Mtukufu wa al Aqsa na kusisitiza kuwa, makundi ya muqawama na wananchi wa Palestina wako tayari kuulinda Msikiti wa al Aqsa na kuzikomboa ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina.
-
Hamas yautahadharisha utawala haramu wa Israel: Usicheze na moto
May 04, 2022 21:54Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetahadharisha kuhusu vitendo vya kichochezi vya Wazayuni katika Msikiti wa Al-Aqsa na kusema vitendo hivyo ni sawa na kucheza na moto.
-
Balozi wa Palestina London aitaka Magharibi kukomesha unafiki
May 04, 2022 21:51Mwakilishi wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina nchini Uingereza ameashiria kimya cha nchi za Magharibi mbele ya vitendo vya kikatili vinavyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Msikiti wa Al-Aqsa na kueleza kuwa, Palestina itakombolewa kutokana na uungaji mkono mkubwa wa watu huru duniani.