Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyed Ali Khamenei Jumatano alikutana na washiriki wa Mashindano ya 33 ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu ya Iran na kusema, 'Qur'ani Tukufu ni mhimili wa Umoja wa Umma wa Kiislamu.
Vijana kutoka kanda ya Afrika Mashariki ni miongoni mahuffadh na maqari wanaoshiriki duru ya 33 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani inayofanyika hapa mjini Tehran.
Baada ya Dk Ali Larijani, Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) kufungua duru ya 33 ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu jana Jumatano, mashindano hayo yameanza rasmi leo.
Mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al Mustafa (SAW) nchini Senegal amekutana na viongozi wa Wakristo nchini humo na kuwakabidhi zawadi ya nakala ya Qur’ani iliyotarjumiwa kwa lugha ya Kifaransa.