Mar 19, 2024 06:12
Tume Kuu ya Uchaguzi ya Shirikisho la Russia imetangaza kuwa Vladimir Putin, rais wa sasa wa nchi hiyo, ameshinda uchaguzi wa karibuni kwa asilimia 87.32 ya kura na hivyo kupata fursa nyingine ya kuwa rais wa Russia kwa muhula mwingine wa miaka sita. Kwa mujibu wa tangazo la tume hiyo, kiwango cha ushiriki katika uchaguzi kilikuwa cha zaidi ya asilimia 70.