-
Mvutano mpya katika uhusiano wa Russia na Israel baada ya shambulizi dhidi ya uwanja wa ndege wa Damascus
Jun 17, 2022 05:29Uhusiano kati ya Russia na utawala wa Kizayuni wa Israel umeingia katika awamu mpya yenye mivutano baada ya mashambuizi ya Russia dhidi ya Ukraine kutokana na misimamo ya Tel Aviv ya kujiunga na nchi za Magharibi na kuchukua misimamo dhidi ya Russia.
-
Russia: Israel iache mashambulizi dhidi ya Syria au isubiri matokeo mabaya
Jun 13, 2022 05:44Balozi wa Russia nchini Syria amelaani vikali jinai ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kufanya shambulio katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Damascus, mji mkuu wa Syria.
-
Russia yasambaratisha ghala kubwa la silaha za Magharibi nchini Ukraine
Jun 12, 2022 22:45Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa jeshi la nchi hiyo limesambaratisha ghala kubwa la silaha za nchi za Magharibi katika vita vinavyoendelea nchini Ukraine.
-
Russia yalaani shambulio la Israel katika uwanja wa ndege wa Damascus Syria
Jun 11, 2022 02:56Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imelaani jinai ya utawala wa Kizayuni ya kufanya shambulio katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Damascus, mji mkuu wa Syria.
-
Russia: Azimio la IAEA dhidi ya Iran ni la kipumbavu
Jun 10, 2022 21:58Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika taasisi za kimataifa zenye makao yao mjini Vienna, Austria amelitaja azimio lililopasishwa hivi karibuni na Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA dhidi ya Iran kuwa ni la kipumbavu.
-
Russia yaonya kuhusu uwezekano wa makabiliano ya moja kwa moja ya kijeshi na kambi ya Magharibi
Jun 10, 2022 21:53Russia imezionya nchi za Magharibi kuwa hujuma ya kiintaneti dhidi ya miundomsingi yake ni jambo ambalo litaibua hatari ya kutokea makabiliano ya moja kwa moja ya kijeshi. Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imetoa taarifa na kusema kuwa, miundomsingi ya kijeshi na ya baadhi ya taasisi za kiserikali nchini humo imekumbwa na hujuma ya kiintaneti ambayo imetekelezwa na makundi ya wadukuzi wa Marekani na Ukraine.
-
Umoja wa Afrika wataka Russia iondolewe vikwazo
Jun 04, 2022 03:11Vikwazo dhidi ya Russia katika nyanja ya usambazaji wa kimataifa wa nafaka na mbolea vinapaswa kuondolewa, Rais wa Senegal na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika Macky Sall alisema Ijumaa baada ya mazungumzo na Rais wa Russia Vladimir Putin.
-
Medvedev: Russia iko kwenye vita vinavyopiganwa kwa niaba ya Marekani na Ulaya
Jun 03, 2022 23:37Mkuu wa Baraza la Usalama wa Taifa la Russia amesema, nchi yake iko kwenye vita vinavyopiganwa kwa niaba ya Marekani na Ulaya na akasisitiza kuwa kuna ulazima wa kuzuia kutokea vita vya atomiki.
-
Russia yafanya mazoezi ya kijeshi ya nyuklia huku mivutano na Magharibi ikiongezeka
Jun 01, 2022 03:12Duru za habari zimeripoti kuwa vikosi vya atomiki vya jeshi la Russia vimefanya mazoezi ya nyuklia katika eneo lililoko kaskazini mashariki ya mji mkuu wa nchi hiyo Moscow.
-
Umoja wa Ulaya washindwa kuiwekea Russia vikwazo vya mafuta; hitilafu zaongezeka
May 30, 2022 06:32Jitihada za Umoja wa Ulaya za kufikia muafaka kuhusu kutekeleza awamu ya sita ya vikwazo dhidi ya Russia zimegonga mwamba kwani Hungary ni moja ya wapinzani wakubwa zaidi wa mpango huo. Wanadiplomasia wa ngazi za juu wa Umoja wa Ulaya katika kikao chao maalumu cha Jumapili walijadili mpango wa kuzuia meli za mafuta za Russia kuingiza mafuta Ulaya lakini waruhusu mafuta hayo yaingie kwa mabomba. Hata hivyo mazungumzo hayo yalimalizika bila natija.