-
Waholanzi 640 waliohudumu katika jeshi la Israel Gaza kushtakiwa?
Feb 19, 2026 23:56Zaidi ya raia 640 wa Uholanzi wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Gaza na kwneye mashambulizi dhidi ya Ukingo wa Magharibi, takwimu mpya zinaonyesha, huku wataalamu wa sheria wakionya kwamba, wale waliohusika wanaweza kushtakiwa chini ya sheria za kimataifa na za nchi hiyo za uhalifu wa kivita.
-
Zaidi ya raia 2,000 wa UK wamepigana kwa niaba ya Israel katika mauaji ya halaiki Gaza
Feb 12, 2026 22:32Maelfu ya raia wa Uingereza wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Akademia ya Geneva: Waliofariki Ghaza wanakaribia 200,000, watu wamepungua kwa 10%
Feb 07, 2026 22:56Stuart Casey Maslen, mkuu wa Akademia ya Geneva ya Sheria za Kimataifa za Kibinadamu na Haki za Binadamu amesema, tangu Oktoba 2023 hadi sasa, idadi ya watu huko Ghaza imepungua kwa zaidi ya 10%, hali inayoashiria kutokea vifo takribani laki mbili.
-
Guardiola apaza sauti tena kuhusu mauaji ya kimbari ya Ghaza na dhulma inayotawala duniani
Feb 05, 2026 02:35Kocha wa timu ya soka ya Manchester City, Pep Guardiola, amesema mauaji ya watu wasio na hatia duniani kote yanamuathiri sana na amewahimiza walimwengu wasinyamazie kimya dhulma zinazofanywa.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina, yaua 20 Gaza
Feb 04, 2026 06:53Mashambulizi mapya ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamewaua shahidi watu wasiopungua 20, wakiwemo watoto wadogo katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaua Wapalestina 31 wakiwemo watoto 6 katika ukiukaji mpya wa usitishaji vita Ghaza
Jan 31, 2026 11:14Wapalestina wasiopungua 31, wakiwemo kwa uchache watoto sita, wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel tangu alfajiri ya leo hadi wakati huu katika Jiji la Ghaza na mji wa Khan Younis katika Ukanda wa Ghaza.
-
Katika mazungumzo na US, Misri yahimiza Israel iondoke Ghaza, ifungue tena kivuko cha Rafah
Jan 26, 2026 00:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty ametoa wito kwa utawala wa kizayuni wa Israel kujiondoa katika Ukanda wa Ghaza na kufungua tena kivuko cha mpakani cha Rafah kuliingana na makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoanza kutekelezwa Oktoba mwaka jana.
-
Shambulio la droni la Israel laua watoto 2 Gaza
Jan 25, 2026 03:46Watoto wawili wameuawa shahidi katika shambulio la Israel kaskazini mwa Ukanda wa Gaza, katika ukiukaji wa hivi karibuni wa makubaliano ya kusitisha mapigano baina ya utawala huo katili na Harakati ya Muqawama ya Hamas katika eneo hilo la Wapalestina linalokaliwa kwa mabavu.
-
Trump atishia kuiwekea Ufaransa ushuru wa 200% kumshinikiza Macron ajiunge na 'Bodi ya Ghaza'
Jan 20, 2026 23:08Rais wa Marekani Donald Trump amemkosoa vikali Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwa kukataa kujiunga na kile kinachoitwa "Bodi ya Amani" ya Washington kwa ajili ya Ghaza, huku mpango huo ukikabiliwa na ukosoaji mkubwa wa wataalamu wa sheria za kimataifa wanaouelezea kuwa ni upanuzi wa ukaliaji wa mabavu wa eneo hilo la Palestina unaofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Trump auza viti vya 'Bodi ya Amani' Gaza dola bilioni 1
Jan 18, 2026 06:54Rais wa Marekani, Donald Trump amezitaka nchi mbali mbali duniani zilipe angalau dola bilioni 1 ili kusalia katika "Bodi ya Amani" ya Gaza, baada ya kumalizika muhula ulioanishwa wa miaka mitatu.