-
UN: Watu milioni moja huko Myanmar wana hali mbaya
Jun 17, 2021 08:12Umoja wa Mataifa umesema kuwa watu milioni moja wana hali mbaya huko Myanmar na wanahitaji misaada ya haraka ya kimataifa.
-
UN yakosoa mienendo ya vikosi vya usalama vya Jamhuri ya Afrika ya Kati
Jun 17, 2021 02:21Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amewakosoa vikali maafisa usalama wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, kwa kile alichokitaja kuwa kushtadi mienendo ya kiuhasama na vitisho dhidi ya askari wa kulinda amani wa umoja huo nchini humo.
-
Mahakama ya UN yashikilia hukumu dhidi ya Mladic, aliyeua Waislamu 8,000 Bosnia
Jun 08, 2021 22:39Majaji wa Mahakama ya Jinai za Kivita ya Umoja wa Mataifa wamedumisha hukumu ya kifungo cha maisha jela dhidi ya Jenerali Ratko Mladic, aliyekuwa kamanda wa kijeshi wa Serbia, ambaye mwaka 2017 alipatikana na hatia ya kuagiza na kuongoza mauaji ya maelfu ya Waislamu huko Srebrenica mwaka 1995.
-
UN yataka kufanyike uchunguzi kuhusu kaburi la umati la watoto wa wakazi asilia wa Canada
Jun 05, 2021 02:49Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamezitaka Canada na Vatican kufanya uchunguzi kuhusu kaburi la umati lililogunduliwa likiwa na maiti 215 za watoto wa wakazi asilia katika jimbo la British Columbia huko Canada.
-
UN: Waasi wa ADF waua raia 57 mkoani Ituri, Congo DR
Jun 04, 2021 22:02Umoja wa Mataifa umeripoti kuwa waasi wa kundi la ADF tarehe 31 mwezi Mei mwaka huu waliwauwa raia 57 katika kambi za watu wasio na makazi mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu jinai za Israel dhidi ya Wapalestina katika ardhi za mwaka 1948
Jun 04, 2021 21:58Katika ripoti yake mpya, Umoja wa Mataifa umefichua jinai mpya kadhaa zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wanaoishi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel tangu mwaka 1948.
-
Nchi 63 zalitaka Baraza la Haki za Binadamu la UN lichunguze jinai za Israel huko Palestina
May 21, 2021 21:59Nchi 63 zimelitaka Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lifanye uchunguzi na kushughulikia jinai zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya raia wasio na hatiai wa Palestina.
-
BAKWATA lalaani unyama wa Israel, lawataka Waislamu wote Tanzania kuliombea nusra taifa la Palestina
May 20, 2021 09:58Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) limelaani vitendo vya kinyama na uadui vinavyofanywa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa taifa madhulumu la Palestina vikiwemo vya kuua raia wasio na hatia.
-
UN yaiomba Tanzania iwape hifadhi raia wa Msumbiji wa Cabo Delgado wanaokimbia mapigano
May 19, 2021 01:58Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UBHCR limesema lina wasiwasi mkubwa na taarifa zinazoendelea za watu wanaokimbia jimboni Cabo Delgado nchini Msumbiji kurudishwa kwa nguvu baada ya kuvuka mpaka kuelekea nchi jirani ya Tanzania.
-
Katibu Mkuu wa UN: Wapiganaji wa kigeni wangaliko Libya, ni ukiukaji wa usitishaji vita
May 15, 2021 09:17Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema, wapiganaji wa kigeni na mamluki wangali wako nchini Libya, ukiwa ni ukiukaji wa mapatano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwaka jana; na akatoa mwito waondolewe nchini humo na kukomeshwa pia ukiukaji wa vikwazo vya silaha vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa.