-
Israel yakataa pendekezo la UN la kusitisha mashambulizi dhidi ya Wapalestina
May 12, 2021 06:01Duru za Palestina zimeripoti kuwa, utawala haramu wa Israel umekataa pendekezo la mjumbe wa Umoja wa Mataifa la kusitisha mashambulizi mara moja dhidi ya watu wa Palestina.
-
UN: Kundi la Daesh lilifanya jitihada za kuangamiza Waislamu wa madhehebu ya Shia
May 11, 2021 20:17Mkuu wa timu ya Umoja wa Mataifa iliyopewa jukumu la kuchunguza jinai na uhalifu uliofanywa na kundi la kiwahabi la Daesh amesema kuwa, kundi hilo la kigaidi lilifanya jitihada za kuangamiza Waislamu wa madhehebu ya Shia.
-
UN: Kuna ongezeko la hatari kwa watoto nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati
Apr 28, 2021 03:30Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa, UNICEF, nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, amesema watoto 370,000 kwa sasa ni wakimbizi wa ndani nchini kote kwa sababu ya vurugu zinazoendelea na ukosefu wa usalama.
-
Guterres: Magufuli atakumbukwa kwa kurejesha maadili ya utumishi wa umma, kupambana na rushwa
Apr 17, 2021 03:27Baadhi ya viongozi walioshiriki katika kikao cha 75 cha mkutano wa 59 wa Umoja wa Mataifa (UN) uliofanyika jana Ijumaa mjini New York wamebainisha alama za uongozi za rais wa awamu ya tano wa Tanzania, John Magufuli wakishauri kuendelezwa mema aliyoyatenda na kuahidi kushirikiana na Rais wa sasa wa nchi hiyo Samia Suluhu Hassan.
-
Raia 65,000 wahama makazi yao kaskazini mashariki ya Nigeria kukimbia mashambulio ya kundi la ISWAP
Apr 16, 2021 22:12Shirka la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeripoti kuwa, watu wasiopungua 65,000 wameuhama mji wa Damasak kaskazini mashariki ya Nigeria kufuatia mashambulio kadhaa ya kundi la wabeba silaha.
-
UN: Eritrea ikomeshe ukatili na mauaji Tigray
Apr 16, 2021 07:35Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, askari wa Eritrea wanapaswa kukomesha ukatili na vitendo viovu katika eneo la Tigray nchini Ethiopia na kuondoka mara moja katika eneo hilo.
-
Zarif: Kukishambulia kituo cha nyuklia cha Iran ni jinai ya kivita
Apr 13, 2021 02:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kitendo cha Jumapili alfajiri cha kushambuliwa kwa makusudi mfumo wa usambazaji umeme wa kituo cha urutubishaji urani cha kituo cha nyuklia cha Natanz hapa nchini ni jinai ya kivita.
-
Foreign Policy yafichua taasisi bandia inayodai kuwa na uhusiano na UN, inahusishwa na uhalifu wa kimataifa
Mar 24, 2021 22:04Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Foreign Policy umefichua habari za taasisi moja inayodai kuwa na uhusiano na Umoja wa Mataifa na kutetea haki za binadamu ambayo viongozi wake wanatuhumiwa kuhusika na uhalifu na jinai nyingi zikiwemo za kutakatisha fedha chafu na kutorosha mabilioni ya dola za Marekani zilizokuwa zimeporwa kutoroshwa nje ya nchi na kiongozi wa zamani wa Libya, Muammar Gaddafi kabla ya kuuawa kwake.
-
UN: Zaidi ya 200 wameuawa katika mashambulio ya wabeba silaha DRC
Mar 20, 2021 06:06Umoja wa Mataifa umesema watu zaidi ya 200 wameuawa katika mashambulio ya magenge ya wabeba silaha katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo tokea Januari mwaka huu hadi sasa.
-
UN: Vikwazo vya silaha dhidi ya Libya havina athari yoyote
Mar 17, 2021 04:01Wataalamu wa Umoja wa Mataifa wamesema vikwazo vya silaha vya umoja huo dhidi ya Libya vinaendelea kukiukwa na kwa msingi huo havina taathira yoyote.