-
Hizbullah yasema imerusha maroketi dhidi ya kambi ya utawala za Kizayuni wa Israel
Aug 06, 2021 07:14Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa wapiganaji wake wa kituo cha Shahidi Ali Muhsin Kamel na Shahidi Muhammad Qassim Tahal wamejibu mashambulizi ya karibuni ya utawala wa Kizayni wa Israel dhidi ya ardhi ya Lebanon kwa kufurumusha maroketi kadhaa dhidi ya utawala huo.
-
UN yapinga matamshi ya kifidhuli ya utawala wa Israel dhidi ya Iran
Aug 06, 2021 01:46Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amepinga matusi na matamshi ya kifidhuli yaliyotolewa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Msimamo mmoja wa nchi 14 za Afrika wa kupinga utawala wa Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika
Aug 01, 2021 02:15Kanali ya al-Waaqe' ya Algeria ilitangaza Jumamosi kuwa nchi hiyo imeanzisha rasmi mchakato wa kubuni kundi la Kiafrika litakalofuatilia kutenguliwa uamuzi wa kuruhusiwa utawala haramu wa Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika AU, ili kulinda misingi ya umoja huo inayounga mkono taifa la Palestina.
-
Ripoti: Mateka wa kike wa Palestina wanakabiliwa na hali mbaya katika jela za Israel
Jul 31, 2021 03:46Kamati ya Masuala ya Mateka wa Palestina imetangaza kuwa mahabusu na mateka wa kike wa Palestina wanaoshikiliwa katika jela za Israel wanaendelea kusumbuliwa na ukatili na hali ngumu kupita kiasi.
-
Mwanajudo wa Algeria: Nimefurahi kuona hatua yangu imeikasirisha Israel
Jul 30, 2021 03:32Fath-i Nurin, mwanamichezo wa mchezo wa Judo wa Algeria ambaye kwa sababu ya kutokubali kuutambua utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kwa ajili kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina hakuwa tayari kupambana na mshindani kutoka utawala huo katika mashindano ya Olimpiki ya Tokyo 2020, amesema, amefurahia hatua yake hiyo kwa kuwa imeikasirisha Tel Aviv.
-
Afrika Kusini yapinga Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika AU
Jul 28, 2021 22:03Serikali ya Afrika Kusini imepinga kitendo cha kutambuliwa utawala haramu wa Israel kuwa mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika (AU.
-
Wazayuni wakasirika kwa "kususiwa kimichezo" katika mashindano ya Olimpiki ya Tokyo 2020
Jul 27, 2021 22:55Duru za habari za lugha ya Kiebrania zimetangaza kuwa kususiwa wanamichezo wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mashindano ya Olimpiki ya Tokyo 2020 kumewakasirisha na kuwashtusha viongozi wa utawala huo haramu.
-
Kwa msaada wa askari wa Israel, walowezi wa Kizayuni wauvamia tena msikiti wa Al Aqsa
Jul 27, 2021 10:40Walowezi wa Kizayuni waliokuwa wakilindwa na kusindikizwa na askari wa utawala haramu wa Israel leo wameuvamia tena msikiti wa Al Aqsa katika mji mtukufu wa Baitul Muqaddas (Jerusalem).
-
Hizbullah: Israel inafanya uchokozi wa waziwazi dhidi ya ardhi za Syria na Lebanon
Jul 23, 2021 07:13Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imesema, shambulio la karibuni la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Syria ni uchokozi na uvamizi wa waziwazi dhidi ya ardhi ya nchi hiyo na ardhi ya Lebanon.
-
Mataifa ya Kiarabu yakosolewa kwa kunyamazia kimya matukio ya kuhujumiwa msikiti wa al-Aqswa
Jul 18, 2021 06:54Sheikh Ikrima Sabri, Khatibu wa Masjidul-Aqswa amekosoa vikali kimya cha mataifa ya Kiarabu na Kiislamu kuhusiana na matukio ya hujuma na uvamizi dhidi ya msikiti wa al-Aqswa.