-
Jihadul-Islami: Walowezi wa Kizayuni ni walengwa halali wa mashambulio ya wanamuqawama
Jul 17, 2021 03:43Msemaji wa harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina amesisitiza kuhusu haki halali na ya kisheria ya kujihami waliyonayo Wapalestina na akabainisha kwamba, walowezi wa Kizayuni ni walengwa halali kisheria wa muqawama.
-
Rais wa Algeria asisitiza kuangamizwa utawala wa Kizayuni
Jul 15, 2021 06:54Rais wa Algeria jana usiku alifanya mazungumzo ya simu na Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina na kusisitiza kuwa, nchi yake itaendelea kuwa bega kwa bega na Wapalestina hadi kuangamizwa maghasibu Wazayuni na kuundwa dola huru la Palestina.
-
Vyombo vya habari vya Kizayuni: Hizbullah ina makombora 150,000 yafikayo umbali wa kilomita 700
Jul 15, 2021 03:18Vyombo vya habari utawala wa Kizayuni vimekiri kuhusu hatua kubwa iliyopiga harakati ya Hizbullah ya Lebanon katika sekta ya makombora na kueleza kwamba Hizbullah ina makombora laki moja na nusu na endapo yatatokea makabiliano katika siku za usoni itakuwa na uwezo wa kufyatua makombora elfu moja hadi elfu tatu kwa siku kuelekea Israel (Palestina inayokaliwa kwa mabavu).
-
Az-Zahar: Ilicho tayari kutekeleza HAMAS ni kubadilishana "mateka kwa mateka" tu
Jul 12, 2021 03:01Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, katika faili la ubadilishanaji wa mateka, harakati hiyo haitakubali sharti jengine lolote lile na kwamba mateka wa utawala wa Kizayuni wa Israel wataachiwa huru ikiwa tu mateka Wapalestina pia wataachiliwa.
-
Hamas yawataka wakazi wa Ukingo wa Magharibi kudumisha mapambano dhidi ya Wazayuni
Jul 11, 2021 00:12Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imewataka wakazi wa Ukingo wa Magharibi mwa Mto Jordan kudumisha mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na kuhakikisha kwamba ardhi ya Palestina inakuwa kaa la moto kwa maghasibu hao.
-
Mfalme wa Jordan aonana na waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni
Jul 09, 2021 08:08Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimetangaza kuwa, mfalme wa Jordan ameonana na waziri mkuu wa Israel katika mji mkuu Amman.
-
Kukosolewa hatua ya Imarati ya kuwapatia uraia Wazayuni
Jul 06, 2021 06:39Ikiwa ni katika mwendelezo wake wa kuimarisha uhusiano wake na utawala haramu wa Israel, serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) imechukua hatua ya kuwapatia uraia Wazayuni.
-
Jihadul Islami: Tunazo nguvu za kuwatimua Wazayuni katika ardhi zote za Palestina
Jul 03, 2021 22:06Kiongozi wa ngazi za juu wa harakati ya Jihadul Islami ya Palestina amesisitiza kuwa, muqawama wa wananchi wa Palestina una nguvu za kuufurusha kikamilifu utawala wa Kizayuni na walowezi wa Kizayuni katika kila shibri ya ardhi ya Palestina.
-
Syria yaalani misimamo ya Marekani na utawala wa Kizayuni kuhusu Miinuko ya Golan
Jun 27, 2021 21:59Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria kwa mara nyingine tena imesisitiza kuwa eneo la Golan ni sehemu ya ardhi ya nchi hiyo na kueleza kuwa, mamlaka ya nchi hiyo kwa eneo la Golan haibadiliki kwa kupita muda na misimamo ya Marekani na utawala wa Israel haina taathira yoyote ya kisheria.
-
Hamas: Guterres amebariki jinai dhidi ya watoto wa Palestina
Jun 19, 2021 22:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imetangaza kuwa, hatua ya Umoja wa Mataifa ya kutoliweka jina la utawala wa Kizayuni wa Israel katika orodha ya wakiukaji wa haki za watoto ni sawa na kubariki jinai zinazofanywa na utawala huo.