-
Kwa nini Marekani inafanya njama za kuidhibiti Venezuela?
Dec 02, 2025 07:15Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amesisitiza kuwa, nchi yake itaendelea kulinda rasilimali zake kwa nguvu zote mbele ya tamaa ya kuchupa mipaka ya Marekani.
-
Venezuela: Tunathamini uungaji mkono madhubuti wa Iran dhidi ya vitisho vya Marekani
Nov 30, 2025 12:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela amesema nchi yake inathamini kwa dhati uungaji mkono wa Iran kwa nchi hiyo ya Amerika ya Latini mkabala wa vitisho vya kijeshi na mashinikizo ya Marekani.
-
Caracas yamhutubu waziri wa Israel: Jina Venezuela ni kubwa, haliwezi kutamkwa na kinywa chako kichafu
Nov 26, 2025 03:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela ametumia lugha kali kujibu tuhuma za waziri wa mambo ya nje wa utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Caracas, kwa kumwita waziri huyo "mhalifu wa kivita" ambaye iwe sasa hivi au baadaye lazima akawajibishwe mbele ya vyombo vya haki na sheria vya kimataifa.
-
Trump asema siku za Rais Maduro wa Venezuela kuweko madarakani zinakaribia ukingoni
Nov 04, 2025 02:24Katika kile kinachotafsiriwa kama harakati ya kibeberu na ya kuingilia masuala ya ndani ya mataifa mengine, Rais wa Marekani Donald Trump ameashiria kuwa siku za Rais Nicolas Maduro wa Venezuela kuweko madarakani zinakaribia ukingoni, huku mvutano kati ya nchi hizo mbili ukiwa unaongezeka sambamba na Washington kushamirisha kuwepo kwake kijeshi katika eneo la Carribean.
-
Kwa nini UN inayataja mashambulizi ya Marekani katika Bahari ya Karibi kuwa ni kinyume na sheria za kimataifa?
Nov 02, 2025 04:50Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa mashambulizi ya Marekani katika eneo la Caribbean yanakiuka sheria za kimataifa.
-
Je, maafa ya Ghuba ya Nguruwe yatakariri kwa Marekani kuhusiana na mvutano wa sasa na Venezuela?
Oct 26, 2025 02:22Huku uwezekano wa Marekani kuishambulia Venezuela ukiongezeka, kunajitokeza swali kwamba, je hadithi ya Ghuba ya Nguruwe (Bay of Pigs) itakaririwa kuhusiana na Venezuela?
-
NAM yaonya kuhusu chokochoko za Washington; Je, Marekani iko mbioni kushambulia Venezuela?
Oct 19, 2025 02:40Wakati ripoti zikionyesha kuwa Pentagon inatayarisha machaguo ya kijeshi dhidi ya Venezuela, Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM), ambayo inaundwa na zaidi ya nchi 120, imeonya kwamba shambulio lolote dhidi ya nchi hiyo ya Amerika Kusini litakuwa ukiukaji wa wazi wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa.
-
Venezuela yatangaza 'maeneo mapya ya ulinzi' mpaka wa Colombia
Oct 16, 2025 09:41Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro amesisitiza kujitolea kwa taifa lake kwa amani, uhuru na utu, akizindua mpango mpya wa kuimarisha ulinzi wa ardhi ya nchi hiyo, huku Marekani ikiidhinisha operesheni za CIA katika eneo hilo.
-
Balozi: US inaihangaisha dunia kwa kisingizio cha kuleta 'uhuru'
Oct 15, 2025 02:32Balozi wa Venezuela nchini Iran, José Rafael Silva Aponte amesema Marekani inaihangaisha dunia nzima, ikiwa ni pamoja na Amerika ya Kusini, kwa kutumia kisingizio cha kuleta uhuru katika maeneo tofauti ya dunia, lakini Venezuela daima itasalia kuwa nchi huru na yenye mamlaka ya kujitawala.
-
Amerika ya Kusini yagawanyika juu ya kiongozi wa upinzani Venezuela kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel
Oct 12, 2025 05:24Kutunukiwa Tuzo ya Amani ya Nobel kiongozi wa upinzani nchini Venezuela María Corina Machado kumeibua hisia tofauti katika nchi za Amerika Kusini, huku baadhi ya viongozi wa nchi za eneo hilo wakipongeza hatua hiyo na wengine kulaani vikali kwa kuashiria matamshi na vitendo vya Machado vya kuchochea vurugu na machafuko au hata kuunga mkono kufanywa mashambulio na uvamizi wa kigeni dhidi ya nchi yake mwenyewe.