Kuzidi kuharibika uhusiano wa kidiplomasia kati ya India na Canada
India imemfukuza mwanadiplomasia wa Canada ikilipiza kisasi kwa hatua ya Canada kumfukuza mwanadiplomasia wa nchi hiyo. Hii ina maana kwamba, kiwango cha mvutano wa kisiasa na kidiplomasia katika uhusiano wa India na Canada kimeongezeka.
Kitendo cha India cha kumfukuza mwanadiplomasia wa Canada kinaonyesha kuwa, New Delhi haikubaliani na shutuma za Ottawa kwamba India ilihusika katika mauaji ya kiongozi wa Wasikh wanaotaka kujitenga nchini humo. Serikali ya Canada bado inasisitiza kuwa, India ilihusika katika mauaji ya mmoja wa viongozi wa wanaotaka kujitenga katika jimbo la Punjab kwenye ardhi ya nchi hiyo, na kama ishara ya kupinga, imechukua hatua ya kumfukuza mwanadiplomasia wa India. New Delhi imelipiza kisasi dhidi ya hatua ya Ottawa kwa kumfukuza mwanadiplomasia wake.
"Tsu Su Yuzheng", mtaalamu wa masuala ya kimataifa, anasema kuwa: Canada, kama vile nchi nyingine za Ulaya na Marekani imekaribisha nchini humo kundi la Sikh Taliban la wanaotaka kujitenga nchini India ambalo linataka kuunda nchi inayoitwa Khalstan katika eneo la kijiografia la India. Canada inatumia mvutano na mgogoro kati ya pande mbili hizo kama fimbo ya kuishinikizo Delhi New. Wakati huo huo,India inafahamu kuwa muundo wa Canada iko chini ya ufalme wa Uingereza, na Ottawa inatekeleza sera na siasa za mfumo mzima wa ufalme huo.
Siasa hizo zinafuatiliwa kwa karibu sana na serikali ya Canada na Justin Trudeau, Waziri Mkuu ana nafasi muhimu, katika uwanja huo. Shutuma kali za Waziri Mkuu wa Canada dhidi ya India kuhusu kuuawa kiongozi mashuhuri wa Sikh katika jimbo la Punjab zinaonyesha umuhimu kwa Canada wa kuwepo kundi la wanaotaka kujitenga nchini India nchini humo. Kwa hivyo, radiamali kali ya India inaonyesha serikali ya New Delhi haitaruhusu kuchezewa mvutano na mgogoro wa eneo na umoja wa kitaifa wa India na madola ya magharibi.
Kwa upande mmoja, Serikali ya India inawatuhumu wanadiplomasia wa Canada kuingilia kati masuala ya ndani ya India , na hatua ya Wizara ya Mambo ya Nje ya India, ya kumfukuza mwanadiplomasia mkuu wa Canada inaonyesha wasiwasi mkubwa wa India kuhusiana na athari ya siasa zilizo dhidi yake za Ottawa kuhusiana na masula ya ndani ya nchi hiyo.
Deepa MC Singh, mtaalamu wa masuala ya kisiasa, anasema: "India kwa kuwa na dini nyingi tofauti, rangi na lugha tofauti tofauti inahesabiwa kuwa ni yenye umoja na muungano mkubwa wa kitaifa. Lakini nchi za magharibi zinatumia suala la kuunga mkono makundi yanayotaka kujitenga,na kuyakaribisha makundi ya upinzani kama vile la Sikh kama siasa za kuishinikiza serikali ya India. Kwa kuzingatia historia ya Uingereza katika kuitawala India, ni jambo lilo wazi kwamba serikali ya London iko nyuma ya mvutano kati ya India na Canada.
Kwa vyovyote vile, India, huku ikikataa shutuma za Wacanada kuhusu mauaji ya Hardeep Singh Nijjar, mmoja wa viongozi Sikh wanaodai kutenga katika jimbo la Punjab, imemtangaza kuwa gaidi. Kwa hivyo, serikali ya India imeitaka Canada kuyatokomeza na kuchukua hatua dhidi ya makundi ya kigaidi yanayoeneza ghasia India badala ya kuwatia nguvu moyo
Inaonekana kwamba serikali ya Canada imependelea kuwapa himaya makundi yanayotaka kujitenga ya Sikh badala ya kuimarisha ushirikiano wake na New Delhi. Inafaa kuzingatia kuwa Uingereza kama mkoloni mkongwe wa nchi hiyo,wakati wa kuondoka iliacha mizozo ya mipaka , katika eneo la kijiografia la Bara Hindi kama vile kati ya India na Pakistan, na Pakistan na Afghanistan. Mgogoro wa kujitenga kundi la Sikh na siasa za kuundwa dola la Khalstan ni miongoni mwa sera jumla za London za kutaka kujitanua au kuidhoofisha serikali ya New Delhi.