-
Mwanzilishi mwenza aonya: Wikipedia imekuwa chombo cha propaganda cha CIA, taasisi zingine zenye nguvu
Aug 09, 2026 11:02Mwanzilishi mwenza wa Wikipedia, Lawrence Mark Sanger, ameonya kwamba ensaiklopidia hiyo ya mtandaoni imekuwa chombo cha propaganda, akisema Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) na marekebisho yanayofanywa na makampuni mbalimbali kwenye Wikipedia yamedhoofisha sera yake ya kutopendelea upande wowote.
-
Jenerali wa Trump anatafuta njia ya kujiondoa vitani na Iran huku machaguo ya kijeshi ya Marekani yakipungua
Aug 09, 2026 02:54Mkuu wa Majeshi ya Marekani, Jenerali Daniel Caine, amewasihi maafisa wakuu wa utawala wa Trump kutafuta njia ya kupunguza vita na Iran, akionya kwamba ongezeko zaidi la mapigano ya kijeshi haliwezi kupata mafanikio makubwa na kwamba linawaweka wanajeshi wa Marekani na washirika wake katika hatari ya majibu angamizi ya Iran.
-
Russia yashambulia eneo la kutengeneza makombora na ghala la mafuta la Ukraine huko Kyiv
Aug 08, 2026 12:46Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa vikosi vya ulinzi ya nchi hiyo vimeshambulia kituo cha kijeshi na viwanda cha Ukraine kinachotengeneza makombora ya cruise pamoja na ghala la mafuta huko Kyiv.
-
Telegraph: Vita dhidi ya Iran vinaweza vikawa moja ya makosa ya kihistoria
Aug 08, 2026 03:22Gazeti la Telegraph linalochapishwa nchini Uingereza limekiri katika ripoti yake kwamba Marekani na Israel zimeshindwa katika vita, huku Iran ikiwa imeibuka mshindi, na kwamba vita hivi vinaweza kuwa tukio muhimu sana la kupelekea kupungua satua na ushawishi wa Marekani duniani.
-
Katika kumbukumbu ya mwaka wa 81 tangu US ilipoishambulia Hiroshima, UN yataka silaha za nyuklia ziangamizwe
Aug 07, 2026 12:25Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ameonya kuwa dunia inakabiliwa na ongezeko la hatari ya matumizi ya silaha za nyuklia kutokana na kushamiri migawanyiko ya kisiasa, kutokuaminiana na mashindano ya kijeshi.
-
Watetezi wa Palestina washinda katika uteuzi wa wagombea wa Democratic wa uchaguzi wa US
Aug 07, 2026 12:24Matokeo ya uchaguzi wa mashinani wa Marekani wa kuteua wagombea wa Seneti na Baraza la Wawakilishi katika uchaguzi wa Novemba yanaonyesha ushawishi unaoongezeka wa mrengo wa chama cha Democratic unaotaka mabadiliko, ambao umeliweka suala la Palestina kwenye kitovu cha wito wake wa kisiasa.
-
Trump anazidi kuchanganyikiwa kuhusu ulipizaji kisasi wa Iran, amkabili Hegseth kuhusu uhaba wa silaha
Aug 06, 2026 03:51Rais wa Marekani, Donald Trump, amezidi kukatishwa tamaa na kushindwa mara kwa mara kwa mashine ya kivita ya nchi hiyo kutokana na ulipizaji kisasi wa Iran na amemkabili Waziri wa Vita, Pete Hegseth, kuhusu uhaba wa silaha muhimu za Marekani.
-
Ripoti: Marekani inazishinikiza nchi za Afrika kujiondoa ICC au kukabiliwa na madhara
Aug 05, 2026 12:11Utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani unazishinikiza nchi za Afrika kujiondoa katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) na kutishia kuzichukulia hatua, huku Washington ikiongeza kasi ya kampeni yake dhidi ya mahakama hiyo.
-
Hukumu ya kihistoria nchini Uingereza: Kupinga Uzayuni si chuki dhidi ya Wayahudi
Aug 05, 2026 12:03Katika uamuzi wa kihistoria uliotolewa jana Agosti 4, 2026, Mahakama Kuu ya Rufaa ya Ajira ya Uingereza ilikataa rufaa iliyowasilishwa na Chuo Kikuu cha Bristol dhidi ya msomi David Miller, ikithibitisha mfano wa kisheria unaotambua imani za kupinga Uzayuni kuwa ni itikadi ya kifalsafa inayolindwa chini ya Kifungu cha 10 cha Sheria ya Usawa ya Uingereza ya 2010.
-
Vyombo vya habari Ulaya vyafichua mpango wa kifisadi wa Rais wa FIFA na wandani wa Trump
Aug 05, 2026 02:38Jarida la The Times limefichua kiasi kikubwa cha fedha ambazo rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA), Gianni Infantino, angeweka mfukoni iwapo mpango wa kuuza Kombe la Dunia ungetekelezwa.