-
Amir-Abdollahian: Israel imeongeza kasi ya kuporomoka kwake kwa kuwaua watoto na wajukuu wa kiongozi wa HAMAS
Apr 11, 2024 04:25Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema mauaji ya hivi karibuni yaliyofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wanafamilia wa kiongozi wa Hamas yanaongeza kasi ya kuporomoka kusio na shaka kwa utawala huo.
-
HAMAS: Misimamo ya Israel imekwamisha mazungumzo ya Doha
Mar 29, 2024 08:29Mmoja wa viongozi waandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema mazungumzo ya kusimamisha vita katika Ukanda wa Gaza yamegonga mwamba huko Doha, mji mkuu wa Qatar kutokana na misimamo isiyoeleweka ya utawala haramu wa Israel.
-
Kiongozi Mkuu: Ghaza ndiyo mshindi mkuu kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi
Mar 29, 2024 00:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema vikosi vya Muqawama na watu wa Ghaza ndio washindi kwenye medani ya vita na utawala wa Israel mwangamizaji wa kizazi na akasisitiza kwa kusema: kilele cha kuheshimika na kusimama imara watu wa Ghaza na Palestina na kushindwa utawala wa Kizayuni katika vita hivyo vya miezi sita ni tukio na jambo lenye rehma za Mwenyezi Mungu.
-
Marekani yaiwekea vikwazo GAZA NOW kwa tuhuma za kuchangisha fedha za kuisaidia HAMAS
Mar 28, 2024 07:28Wizara ya Fedha ya Marekani imeiwekea vikwazo tovuti ya mtandao ya GAZA NOW kwa madai ya kuchangisha misaada ya kifedha kwan ajili ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Haniya: Azimio la Baraza la Usalama linaonesha Israel imetengwa duniani
Mar 27, 2024 04:10Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema utawala wa Kizayuni wa Israel umetengwa vibaya na dunia kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa; siku moja baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupasisha azimio la kutaka kusitishwa mara moja mapigano huko Gaza.
-
"Hakuna mwanachama wa HAMAS aliyekamatwa katika Hospitali ya al-Shifa"
Mar 22, 2024 08:16Afisa usalama wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amepuuzilia mbali madai ya utawala haramu wa Israel kwamba makumi ya wanachama wa kundi hilo la mapambano ya Kiislamu wamekatwa na askari wa Kizayuni katika Hospitali ya al-Shifa katika Ukanda wa Gaza.
-
HAMAS: Muqawama wa kupambana na Israel umevuka mipaka ya Ghaza
Mar 18, 2024 07:43Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema utawala wa Kizayuni wa Israel unakabiliwa na "safu pana zaidi" ya Muqawama iliyovuka mpaka wa Ukanda wa Ghaza.
-
AFP: Viongozi wa harakati za muqawama wamekutana kuratibu mashambulizi dhidi ya Israel
Mar 16, 2024 22:43Harakati ya Muqawama za Hamas, Jihad Islami, Harakati ya Wananchi ya Ukombozi wa Palestina na harakati ya Ansarullah ya Yemen zimefanya mkutano kwa ajili ya kuratibu na kuweka mikakati ya pamoja ya kuliunga mkono na kulitetea taifa linalodhulumiwa la Palestina dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
HAMAS yakanusha madai ya kukubali pendekezo la usitishaji vita
Mar 13, 2024 04:15Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imekadhibisha ripoti ya shirika la habari la al-Arabiya kwamba kundi hilo la muqawama limeafiki 'pendekezo la kimataifa' la usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Intelijensia ya Marekani: HAMAS itaendelea kutoa changamoto kwa Israel kwa "miaka kadhaa"
Mar 12, 2024 23:16Ripoti ya tathmini ya kiintelijensia iliyotolewa na Marekani imetilia shaka uwezo wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuifuta Hamas, harakati hiyo ya muqawama ya Palestina huenda ikatoa changamoto "ya muda mrefu" kwa miaka kadhaa kwa utawala huo ghasibu unaokalia ardhi za Palestina kwa mabavu.