-
Wabunge Iraq waitaka serikali ijibu mapigo kwa kutowapatia viza raia wa Imarati
Nov 27, 2020 08:33Baada serikali ya Imarati kusitisha utoaji viza kwa raia wa Iraq wanaotaka kuingia nchini humo, sambamba na kuwaweka kizuizini katika mazingira ya kutatanisha Wairaqi kadhaa wanaoishi nchini humo, wabunge wa Iraq wameitaka serikali yao isitishe kutoa viza kwa raia wa Imarati pia wanaotaka kuingia nchini humo.
-
Afisa wa UAE akiri nchi hiyo imekuwa na uhusiano wa siri na Israel tangu miaka kadhaa nyuma
Nov 22, 2020 00:43Mkuu wa usalama wa mitandao wa serikali ya Imarati amekiri kuwa, kwa miaka kadhaa, nchi hiyo imekuwa na ushirikiano na mashirika ya usalama wa mitandao ya intaneti ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Tangazo la biashara la shirika la ndege la UAE lapotosha jina la Msikiti wa Al Aqsa
Nov 17, 2020 02:07Shirika la ndege la taifa la Umoja wa Falme za Kiarabu limepotosha jina la msikiti wa Al Aqsa katika filamu ya tangazo la biashara lililotoa kutangaza safari zake kuelekea ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina zilizopewa jina la Israel.
-
Imarati yaipa Sudan mamilioni ya dola baada ya kuanzisha uhusiano na Israel
Oct 28, 2020 04:18Umoja wa Falme za Kiarabu umeipa Sudan msaada wa dola nusu bilioni za Marekani, siku chache baada ya Khartoum kukubali kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Madai ya kukaririwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kinyume cha ukweli wa mambo
Oct 23, 2020 04:19Anwar Gargash Waziri Mshauri wa Mambo ya Nje katika Umoja wa Falme za Kiarabu ametuma ujumbe kupitia ukurasa wake wa Twitter na kudai kuwa, Iran inavuruga uthabiti katika eneo la Asia Magharibi.
-
Waziri Mkuu wa Palestina: Inasikitisha kuona Wapalestina wanazuiwa kuswali Masjidul Aqsa huku Waimarati wakiruhusiwa kuingia eneo hilo
Oct 19, 2020 12:05Waziri Mkuu wa Palestina amesema kuwa kitendo cha kuruhusiwa ujumbe wa Imarati kuingia ndani ya Msikiti wa al Aqsa huku Wapalestina wakizuiwa kuswali katika msikiti huo, kinauma sana.
-
Imarati yasema Wapalestina hawana shukrani kwa kukosoa uhusiano na Israel
Oct 15, 2020 04:38Afisa mmoja wa ngazi za juu wa Umoja wa Falme za Kiarabu amewashutumu vikali wananchi wa Palestina na kudai kuwa hawana shukrani wala hawatambui fadhila, kutokana na hatua yao ya kupinga hatua ya Imarati ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Meli ya mizigo ya Imarati yatia nanga katika bandari ya Israel
Oct 13, 2020 04:31Meli ya mizigo ya Umoja wa Falme za Kiarabu imetia nanga katika mji wa bandari wa Haifa, katika maeneo ya Wapaestina yanayokaliwa kwka mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Imarati na Israel; upotoshaji mambo katika kivuli cha kuanzisha migogoro Asia Magharibi
Oct 01, 2020 03:56Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel wamelitumia jukwaa la kila mwaka la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kutoa tuhuma za kukakariwa na zisizo na jipya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Imarati yafanya biashara na mashirika ya Kizayuni yaliyoko kwenye orodha nyeusi ya UN
Sep 24, 2020 23:03Mashirika kadhaa ya Umoja wa Falme za Kiarabu UAE yamesaini mkataba wa ushirikiano na mashirika na makampuni ya Kizayuni yaliyoko kwenye orodha nyeusi ya Umoja wa Mataifa kwa kuunga mkono ujenzi haramu wa vitongoji vya walowezi wa Kizayuni.