-
Iran yaitumia salamu za rambi rambi serikali ya Afrika Kusini kufuatia mlipuko wa lori la gesi
Dec 26, 2022 00:50Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za pole na rambi rambi kwa serikali na wananchi wa Afrika Kusini kufuatia mlipuko wa lori la gesi ambao umesababisha vifo vya watu kadhaa.
-
Iran na Guinea kupanua ushirikiano wao katika kilimo
Dec 24, 2022 02:44Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Guinea zimeazimia kuimarisha zaidi uhusiano wa pande mbili katika sekta ya kilimio ikiwa ni katika mkakati wa Iran wa kuendelea kuboresha zaidi ushirikiano na nchi za Afrika.
-
Iran yapongeza misimamo ya Namibia ya kuliunga mkono taifa la Palestina
Nov 25, 2022 06:37Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu amesifu misimamo ya Namibia ya kuliunga mkono taifa la Palestina na kusisitizia malengo ya pamoja ya Tehran na Windhoek.
-
Iran na Afrika Kusini zaazimia kuimarisha uhusiano wa pande mbili
Nov 17, 2022 04:14Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Afrika Kusini wamesisitizia haja ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili wa nchi hizi mbili katika nyuga tofauti.
-
Mabaharia 16 Wairani waachiliwa huru Tanzania
Nov 13, 2022 01:16Mabaharia 16 Wairani waliokuwa wanashikiliwa nchini Tanzania wameachiliwa huru hivi karibuni. Hayo yamedokezwa na Mkuu wa Ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran katika Eneo la Biashara Huria la Chabahar katika mkoa wa Sistan na Baluchestan kusini-mashariki mwa Iran ambaye amesema mabaharia hao walioachiliwa huru ni wenyeji wa mkoa wa Sistan na Baluchestan.
-
Uhusiano wa Zanzibar na Iran unazidi kuimarika + SAUTI
Oct 20, 2022 13:08Meya wa jiji la Zanzibar ameonana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jijini Dar es Salaam Tanzania na pande mbili zimehimiza mno kuendelezwa uhusiano wa damu na wa jadi baina yao. Harith Subeit na maelezo zaidi kutoka Zanzibar
-
Kumbukumbu za kuuawa shahidi Imam Ridha AS zafanyika nchini Mauritius
Sep 27, 2022 07:22Programu maalumu ya kukumbuka siku alipouawa shahidi Imam Ridha AS zimefanyika nchini Mauritius na kuhudhuriwa na masheikh wawili kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kwa uratibu wa ubalozi wa Iran nchini Madagascar na Kitengo cha Kimataifa cha Haram ya Imam Ridha AS.
-
"Magharibi inafanya njama za kufuta matukufu ya Kiislamu na kupandikiza upotofu wake"
Sep 27, 2022 07:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amendelea na harakati zake za kidiplomasia pembeni mwa kikao cha 77 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa kuonana na kufanya mazungumzo na mawaziri wenzake wa mambo ya nje kuanzia wa mashariki hadi magharibi mwa Asia na kutoka Amerika ya Latini hadi Ulaya na Afrika.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran aonana na mawaziri wenzake wa Uganda, Eritrea na Imarati
Sep 25, 2022 03:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana alionana kwa nyakati tofauti na mawaziri wenzake wa mambo ya nje wa Uganda, Eritrea na Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na kubadilishana nao mawazo kuhusu masuala ya kieneo na kimataifa. Mazungumzo ya mawaziri hao yamefanyika mjini New York, Marekani.
-
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yasikitishwa na machafuko mapya ya Libya
Aug 28, 2022 06:12Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran ameelezea kusikitishwa sana na machafuko mapya ya nchini Libya na ametaka kukomeshwa mara moja mapigano hayo. Amesema, Tehran inazitaka pande hasimu kuzingatia maslahi ya taifa, usalama wa wananchi na kutatua mambo yao kwa njia ya mazungumzo.