-
Mkuu wa zamani wa haki za binadamu wa UN kuongoza uchunguzi wa jinai za Israel
Jul 23, 2021 03:22Baraza la Haki za Binadamu limemteua Navi Pillay, aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kuongoza kamati ya kimataifa ya watu watatu ya kuchunguza jinai za kivita za hivi karibuni za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Israel yawatia mbaroni wanachama zaidi ya 120 wa Hamas katika Ukingo wa Magharibi
Jul 22, 2021 22:03Televisheni moja ya Kizayuni inayotangaza kwa lugha ya Kiibrania imetangaza kuwa Israel miezi miwili iliyopita iliwatia mbaroni wanachama zaidi ya 122 wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) katika Ukingo wa Magharibi mwa Mto Jordan.
-
Snowden: Si ajabu kwamba programu ya kijasusi ya Israel imetumiwa kudukua simu ya Joe Biden
Jul 22, 2021 03:11Mfichuaji maarufu wa kashfa mbalimbali za ujasusi wa Marekani amesema kuwa, si ajabu kusikia kwamba, programu ya ujasusi ya kampuni ya Israel imetumiwa kudukua simu ya mkononi ya Rais Joe Biden.
-
Umoja wa Ulaya: Kashfa ya ujasusi unaofanywa na Israel haikubaliki kabisa
Jul 19, 2021 21:51Mkuu wa Kamisheni ya Ulaya amesema kuwa, kashfa ya hivi karibuni ya ujasusi uliofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel inakinzana na sheria zote za Umoja wa Ulaya.
-
Licha ya kauli kali zitolewazo dhidi ya Wazayuni, marais wa Uturuki na Israel wataka kustawishwa uhusiano
Jul 15, 2021 03:42Chama tawala nchini Uturuki cha Uadilifu na Maendeleo AKP kimesema, Uturuki na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel zimekubaliana kuchukua hatua ili kustawisha uhusiano wao wenye mivutano kufuatia mazungumzo yaliyofanywa kwa njia ya simu kati ya marais wa pande hizo mbili.
-
Jihad al Islami: Muqawama ndiyo njia pekee ya kupambana na Israel
Jul 12, 2021 22:06Msemaji wa Harakati ya Jihad al Islami ya Palestina amewapongeza wanamapambano wa Palestina wanaojihami kwa silaha mbele ya jinai za Wazayuni katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kusema kuwa, hiyo ndiyo njia pekee ya kupambana na Israel.
-
Matunda ya kuonyesha muqawama; kuachiwa huru mateka Mpalestina baada ya kususia kula kwa siku 65
Jul 09, 2021 21:58Mateka Mpalestina, aliyesusia kula kwa muda wa siku 65 akilalamikia kurefushwa hukumu haramu ya kuwekwa kizuizini kiidara iliyotolewa na utawala dhalimu wa Kizayuni wa Israel dhidi yake, hatimaye ameachiliwa huru.
-
Zaidi ya wasomi, wanafikra 600 wa kimataifa wataka kuvunjwa utawala wa kibaguzi katika Palestina ya kihistoria
Jul 07, 2021 23:49Idadi kubwa ya wasomi, wasanii na wanafikra kutoka nchi nyingi duniani wametoa wito wa kuvunjwa mfumo wa ubaguzi wa rangi ulioanzishwa katika ardhi za Palestina ya kihistoria, na kuanzishwa mfumo wa utawala wa kidemokrasia ambao utatoa haki na majukumu sawa kwa wakazi wote wa nchi hiyo bila ubaguzi wowote kwa misingi ya rangi, mbari, dini au jinsia.
-
Hamas: Vitisho vya Gantz ni kwa ajili ya kuboresha sura ya jeshi la Israel
Jul 05, 2021 22:05Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa, vitisho vilivyotolewa na Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel vya kulishambulia tena eneo la Ukanda wa Gaza ni jaribio la kuboresha sura ya jeshi la utawala huo iliyoharibika baada ya kipigo cha karibuni cha wanamapambano wa Kipalestina.
-
Jihad Islami yalaani hatua ya Imarati ya kuwapa uraia Wazayuni 5,000
Jul 05, 2021 07:58Harakati ya Jihad Islami ya Palestina imelaani hatua ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ya kuwapa uraia Wazayuni 5,000 wa Israel ikisema hatua hiyo ni fedheha na aibu nyingine kwa "serikali ya kisaliti ya Abu Dhabi iliyofanya mapatano na utawala katili wa Israel.