-
Madai ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumaini kuhusu JCPOA
May 27, 2019 22:42Umoja wa Ulaya na troika ya umoja huo inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza daima imekuwa ikidai kuwa inaunga mkono mapatano ya nyuklia na Iran maarufu kwa jina la JCPOA na kwmba nchi hizo zimekuwa zikisisitizia muda wote umuhimu wa kutekelezwa kivitendo mapatano hayo.
-
Rais Rouhani: Iran bila shaka itapata ushindi katika makabiliano na Marekani
May 26, 2019 01:50Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria mashinikizo ya kisiasa na kiuchumi ya Marekani dhidi ya Iran ya Kiislamu na kusema: "Taifa la Iran halijawahi na halitasalimu amri mbele ya mashinikizo."
-
Takht-Ravanchi: Marekani ilikiuka wazi sheria za kimataifa kwa kujiondoa JCPOA
May 25, 2019 02:20Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kujiondoa Marekani katika mpatano ya nyuklia ya JCPOA ni ukiukwaji wa wazi wa sheria za kimataifa hasa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Matusi ya Trump dhidi ya taifa la Iran, mgongano katika misimamo ya Washington
May 24, 2019 23:02Baada ya kuingia Ikulu ya White House mnamo mwezi Januari 2017, Rais Donald Trump wa Marekani bila kupoteza wakati ilichukua msimamo wa kudhoofisha na ikiwezekana kuuangusha mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Sisitizo la viongozi wa Russia, Ujerumani na Ufaransa la kulindwa mapatano ya JCPOA
May 22, 2019 05:18Mapatano ya nyuklia yanayojulikana kwa jina la JCPOA yalifikiwa mwezi Julai 2015 mjini Vienna Austria baina ya Iran na kundi la 5+1 lililojumuisha nchi za Marekani, Uingereza, Ufaransa, Russia, China pamoja na Ujerumani na Umoja wa Ulaya. Mapatano hayo yalianza kutekelezwa mwezi Januari 2016.
-
Russia, Ujerumani na Ufaransa zasisitiza kuwa JCPOA lazima ilindwe
May 22, 2019 03:46Viongozi wa Russia, Ujerumani na Ufaransa wamesisitizia haja ya kubakishwa hai na kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, huku wakibainisha kuwa nchi zao zinafanya kila linalowezekana kuimarisha uhusiano wao wa kibiashara na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, licha ya Marekani kuchukua hatua ya upande mmoja ya kujiondoa kwenye mapatano hayo ya kimataifa.
-
Sisitizo la Ujerumani la kutokuwa na natija siasa za "mashinikizo ya kiwango cha juu zaidi" za Donald Trump dhidi ya Iran
May 19, 2019 02:34Rais Donald Trump wa Marekani iwe ni katika kipindi cha kampeni zake za uchaguzi au baada ya kuingia katika ikulu ya White House Januari 2017, ametanguliza mbele mkondo wa siasa za kutaka kuudhoofisha na kuuangusha mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Sisitizo la Rais Putin la kuwa wazi kusiko na mithili miradi ya nyuklia ya Iran
May 16, 2019 21:59Makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) yalitiwa saini Julai 2015 huko Vienna Austria kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kundi la 5+1.
-
Safari ya Pompeo Russia: Jitihada zilizofeli za kupunguza hitilafu baina ya Washington na Moscow
May 15, 2019 22:04Uhusiano wa Marekani na Russia katika zama za baada ya vita baridi umekumbwa na pandashuka nyingi sana. Pamoja na hayo mgogoro wa Ukraine mwaka 2014, na baada ya hapo, yaani katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, uhusiano wa Moscow na Washington umechukua mkondo wa kuzorota na hali imekuwa mbaya zaidi baada ya Marekani kuiwekea Russia vikwazo.
-
Mkutano wa Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Ulaya na sisitizo la kutekelezwa makubaliano ya JCPOA
May 14, 2019 21:47Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya (Ujerumani, Ufaransa na Uingereza) daima zimekuwa zikiunga mkono makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kusisitiza kutekelezwa kwake.