-
Federica Mogherini: Hatua ya kwanza ya mfumo wa INSTEX itaanza wiki chache zijazo
May 14, 2019 00:00Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Bi Federica Mogherini sambamba na kusisitiza juu ya Umoja wa Ulaya kufungamana na utekelezeaji wa mapatano ya nyuklia JCPOA, ameonyesha matumaini kwamba hatua ya kwanza ya mfumo maalumu wa kifedha wa Ulaya na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (INSTEX) itaanza kutekelezwa wiki chache zijazo.
-
Kharrazi: Madola ya Ulaya yanapaswa kuonyesha 'irada' ya kulindwa makubaliano ya JCPOA
May 12, 2019 23:08Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Uhusiano wa Nje la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, madola ya Ulaya yanaweza kuonyesha nia na irada yao ya kutaka kuhifadhiwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA kwa kutekeleza ahadi zake kama kutekelezwa haraka mfumo maalumu wa kifedha wa Ulaya na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (INSTEX).
-
HAMAS: Uamuzi wa Iran kuhusu JCPOA ni wa kishujaa
May 10, 2019 21:48Mwakilishi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina (HAMAS) nchini Lebanon amesema kuwa, hatua ya Iran ya kusitisha kwa muda utekelezaji wa ahadi zake katika baadhi ya vipengee vya mapatano ya nyuklia ya JCPOA, inaonyesha kuwa ni maamuzi ya kishujaa.
-
Taarifa ya Ulaya kuhusu hatua ya Iran; ulazima wa kutekelezwa ahadi badala ya kudhihirishwa masikitiko
May 10, 2019 21:46Baada ya Marekani kutangaza kujitoa katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia, JCPOA, mnamo tarehe 8 Mei mwaka uliopita, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilitaraji kwamba kundi la 4+1 na hasa troika ya Ulaya na Umoja wa Ulaya, lingechukua hatua za kupunguza madhara ya Marekani kuanza kutekeleza tena vikwazo vya nyuklia dhidi ya Iran.
-
Wairan waandamana nchi nzima kuunga mkono hatua za nchi yao kuhusu mapatano ya JCPOA
May 10, 2019 09:00Wananchi wa Iran ya Kiislamu leo Ijumaa wameandamana nchi nzima kuunga mkono hatua zilizochukuliwa humu nchini za kusimamisha utekelezaji wa baadhi ya ahadi za Tehran katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Ulaya na Marekani zaendelea kukosoa hatua za Trump dhidi ya mapatano ya JCPOA
May 09, 2019 23:28Wanasiasa na waharakati wa makundi ya kiraia barani Ulaya na nchini Marekani wameendelea kukosoa hatua za White House dhidi ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran, hatua ya 'mashinikizo ya kiwango cha juu zaidi'
May 09, 2019 23:26Baada ya Rais Donald Trump wa Marekani kutangaza kuiondoa nchi hiyo katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA mnamo tarehe 8 Mei mwaka uliopita, alianza kutekeleza vikwazo vya nyuklia dhidi ya Iran katika hutua mbili yaani mwezi Agosti na Novemba mwaka huo huo.
-
Radiamali ya Umoja wa Ulaya kuhusu maamuzi ya Iran, matarajio ya kulindwa JCPOA bila kutolewa fursa
May 09, 2019 02:47Mapatano ya nyuklia maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA yalifikiwa mjini Vienna mwezi Julai 2015 kati ya Iran na kundi la 5+1, huku utekelezaji wake ukiwa ulianza mwezi Januari 2016.
-
China, Russia, Ufaransa na Ujerumani zatoa radiamali zao kufuatia tangazo la Iran
May 08, 2019 09:20Russia, China, Ufaransa na Ujerumani ambazo ni katika nchi tano zilizosalia katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA zimetoa radimali kufuatia uamuzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kusimamisha kwa muda utekelezaji wa baadhi ya ahadi zake kuhusu mapatano hayo, ikiwa ni mwaka mmoja baada ya Marekani kujitoa kwa upande mmoja katika mapatano hayo muhimu ya kimataifa.
-
Larijani: Hatua zinazochukuliwa na Marekani dhidi ya Iran zinaonesha kuchanganyikiwa Washington
May 05, 2019 03:08Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amesema kuwa hatua zinazochukuliwa na Marekani dhidi ya Iran zinaonesha kuchanganyikiwa viongozi wa nchi hiyo na hawajui cha kufanya.