-
Maveterani wa kivita Marekani wamtaka Trump aombe radhi kwa kudharau hasara kubwa iliyosababishwa na kipigo cha Iran
Jan 26, 2020 03:20Kundi moja la maveterani wa vita vya nje ya Marekani wamemtaka rais wa nchi hiyo Donald Trump aombe radhi kwa kudharau madhara waliyopata wanajeshi wa Marekani baada ya kambi yao ya Ain al Assad ya nchini Iraq kushambuliwa kwa makumi ya makombora ya Iran.
-
Dakta Zarif: Hatua ya madola ya Ulaya ya kuitii kibubusa Marekani ni maafa
Jan 26, 2020 02:54Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hatua ya madola ya Ulaya ya kuitii kibubusa Marekani ni maafa na kueleza kwamba, madola ya ulaya hayana ubavu wa kumpinga Rais Donald Trump wa Marekani.
-
Wamarekani waunga mkono mpango wa kumshtaki Trump ICC
Jan 25, 2020 11:39Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni nchini Marekani unaonesha Wamarekani wanaunga mkono mpango wa kushtakiwa rais wa nchi hiyo, Donald Trump kwa kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani.
-
Marekani na ugaidi wa kiserikali; tishio la kumuua kigaidi kamanda mpya wa kikosi cha Quds cha IRGC
Jan 25, 2020 03:13Baada ya jinai ya Marekani ya kumuua kinyume cha sheria na kiuwoga Luteni Jenerali Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu na Abu Mahdi al Muhandis, Naibu Kamanda wa kikosi cha kujitolea cha wananchi wa Iraq maarufu kama al Hashd al Shaabi pamoja na watu wengine wanane mnamo Januari 3 2020 katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Baghdad, sasa utawala wa Trump umetoa tishio jipya la ugaidi.
-
Iran: Kibao cha uso tulichompiga Mmarekani kitabakia milele katika historia
Jan 24, 2020 08:03Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, athari za kibao kikali cha uso ambacho vikosi vya ulinzi vya Iran vimeipiga Marekani, zitabakia milele katika historia.
-
Ulinzi mkali Iraq sambamba na kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kuifukuza Marekani
Jan 24, 2020 08:01Duru za usalama za Iraq zimetangaza habari ya kuwekwa ulinzi mkali katika kona zote za nchi hiyo ya Kiarabu hasahasa Baghdad kufuatia kuanza maandamano ya milioni ya watu ya kushinikiza kufukuzwa wanajeshi wa Marekani nchini humo.
-
Iran: Marekani imedhihirisha sura yake ya kigaidi kwa kutishia kumuua Brigedia Qaani
Jan 24, 2020 02:53Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali matamshi ya kijuba yaliyotolewa na "kundi la kuichukulia hatua Iran" la wizara ya mambo ya nje ya Marekani ya kutishia kumuua kigaidi Brigedia Jenerali Ismael Qaani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Matokeo hasi ya chokochoko za Marekani Asia Magharibi
Jan 24, 2020 02:52Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa hatua na chokochoko za kijeshi zinazofanywa na Marekani katika eneo la Asia Magharibi, ndio chanzo cha machafuko ndani ya eneo hilo na ameongeza kuwa, uthibitisho wa mwisho wa jambo hilo ni kumuua kigaidi Luteni Qassem Soleimani katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Baghadad, Iraq.
-
Madai ya kijuba ya Marekani kuhusu kamanda mpya wa kikosi cha Quds Brig. Jen. Qaani
Jan 23, 2020 11:36Mwakilishi maalumu wa Marekani katika masuala ya Iran ametoa matamshi ambayo yanaashiria utambulisho wa kigaidi wa serikali ya Washington ambapo amezungumza kuhusu hatua tarajiwa dhidi ya kamanda aliyechukua nafasi ya Shahidi Luteni Jenerali Qasem Soleimani.
-
Mexico yatupilia mbali tuhuma za Marekani dhidi ya Iran
Jan 19, 2020 02:57Wizara ya Mambo ya Nje ya Mexico imetupilia mbali madai ya hivi karibuni ya gazeti la Kimarekani la Wall Street Journal kuhusiana na upenyaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika eneo la Amerika ya Latini.