-
Warepublican waanza mchakato wa kumuondoa Ilhan Omar katika Kamati ya Mambo ya Nje ya Congresi kwa kuikosoa Israel
Feb 02, 2023 08:41Wanachama wa Republican katika Baraza la Wawakilishi la Marekani wanajiandaa kupigia kura muswada wa kumuondoa mwakilishi wa Kidemokrati, Ilhan Omar kwenye Kamati ya Masuala ya Kigeni, siku chache baada ya kuondolewa katika Kamati ya Masuala ya Afrika, kutokana na kukosoa ukatili na mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya raia wa Palestina.
-
Majibu makali ya Tehran kuhusu msimamo ulio dhidi ya Tehran wa Blinken
Feb 01, 2023 22:42Nasser Kan'ani, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, siku ya Jumatatu alijibu upayukaji mpya wa baadhi ya viongozi wa Marekani na kusema kuwa, serikali ya Washington inaelewa vilvyo kwamba Iran haiwezi kufumbia macho uchokozi wa aina yoyote ile wa ardhi yake na lazima itatoa majibu makali kwa yeyote anayelichokoza taifa hili la Kiislamu.
-
Kukosoa Mbunge wa Kiislamu kuhusu kuenea chuki dhidi ya Uislamu katika Kongresi ya Marekani
Jan 31, 2023 22:55Ilhan Omar, Mbunge Mwislamu wa chama cha Democratic katika Baraza la Wawakilishi la Marekani anayewakilisha jimbo la Minnesota amesema kuwa, baadhi ya wajumbe wa chama cha Republican hawataki kuona kunakuweko na Wabunge Waislamu katika Kongresi ya nchi hiyo.
-
Iran: Hatubabaishwi na bwabwaja na matamshi ya vitisho ya Marekani
Jan 30, 2023 23:24Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imekosoa porojo na matamshi ya vitisho ya Marekani na kuonya kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itatoa jibu kali kwa hatua yoyote ya uvamizi dhidi ya taifa hili.
-
Mauaji ya kikatili ya raia mwingine mweusi; ukatili usio na mwisho wa polisi wa Marekani
Jan 29, 2023 04:48Siku ya Ijumaa na baada ya kuchapishwa picha za kutisha za kupigwa kinyama Tyre Nichols, Mmarekani mweusi mwenye umri wa miaka 29 na polisi huko Memphis, katika jimbo la Tennessee, wimbi jipya la maandamano limeanza nchini humo na hasa katika miji ya Memphis, Boston, Chicago, Detroit, New York City, Portland, Oregon na Washington dhidi ya ukatili unaofanywa na polisi dhidi ya watu weusi.
-
Jenerali Mmarekani atabiri vita na China mwaka 2025, anawaambia maafisa wajitayarishe
Jan 28, 2023 23:06Jenerali wa nyota nne wa Jeshi la Wanahewa la Marekani ameonya kuhusu uwezekano wa kutokea mzozo wa kijeshi kati yake na China kuhusu eneo la Taiwan mapema mwaka 2025, na hivyo amewataka makamanda kushinikiza vikosi vyao kufikia utayari wa juu zaidi kwa operesheni za kijeshi.
-
Israel yaufyata baada ya onyo la Russia, yakataa ombi la US la kuipa Ukraine makombora
Jan 26, 2023 23:18Utawala haramu wa Israel umepinga ombi la Marekani la kuutaka uipe Ukraine makombora na silaha nyinginezo, baada ya Russia kuonya vikali dhidi ya kupewa Kiev misaada ya kijeshi na zana za vita.
-
Kan'ani: SEPAH imesambaratisha mikakati ya kibeberu ya Marekani
Jan 26, 2023 00:32Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) limesambaratisha njama za maadui hasa Marekani katika ukanda huu na kuufedhehesha utawala wa Kizayuni.
-
Utafiti: Marekani haipo tayari kuingia vitani na China
Jan 24, 2023 23:00Kituo cha Kimataifa cha Tafiti za Kistratejia (CSIS) kimeonya kuwa, Marekani haina ubavu wala akiba ya kutosha ya silaha na zana za kijeshi za kuiwezesha kuingia katika makabiliano ya kijeshi na China.
-
Watu 10 wauawa kwa kupigwa risasi kwa umati California, Marekani
Jan 23, 2023 01:29Zaidi ya watu kumi wameuawa kwa kupigwa risasi kwa umati huko Monterey Park, California nchini Marekani wakati sherehe za Mwaka Mpya wa Kichina.