-
Russia yaitaka Marekani iache kujifanya 'polisi wa dunia'
Oct 20, 2020 04:29Russia imeikosoa vikali Marekani kwa kufuata tena mkondo ghalati wa kuzishinikiza nchi za dunia zifuate sera, matakwa na maagizo yake.
-
Sudan yakubali kuipa Marekani dola milioni 335 iondolewe katika orodha ya ugaidi
Oct 20, 2020 04:09Rais Donald Trump amesema Marekani itaiondoa Sudan katika orodha ya nchi 'zinazounga mkono ugaidi' baada ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kukubali kuipa Washington dola milioni 335.
-
Hatami, Iran inakidhi asilimia 90 ya mahitaji yake ya kijeshi
Oct 19, 2020 04:09Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran vimekuwa chanzo cha nchi hii kustawi na kujitosheleza katika sekta ya ulinzi. Ameongeza kuwa: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo inaweza kuzalisha ndani ya nchi asilimia 90 ya mahitaji yake yote ya kijeshi.
-
Malalamiko ya wanawake dhidi ya Trump na mustakbali wa rais huyo wa Marekani
Oct 19, 2020 02:47Katika siku zilizopita, wanawake nchini Marekani walifanya maandamano katika majimbo mbalimbali ya nchi hiyo likiwemo la Washington ili kutangaza upinzani wao kwa siasa za rais wa nchi hiyo, Donald Trump. Shabaha ya maandamano hayo ilikuwa ni kupinga ubaguzi wa rangi na ukandamizaji dhidi ya wanawake. Waendeshaji wa maandamano hayo waliahidi kuendelea na operesheni hiyo waliyoipa jina la maandamano 429 katika mikoa 50 ya Marekani.
-
Kukiri mshauri wa usalama wa taifa wa Marekani malengo halisi ya Washington dhidi ya Iran
Oct 18, 2020 23:00Tarehe 8 Mei 2018 Marekani chini ya utawala wa Donald Trump, ilijitoa kwenye mapatano ya kimataifa ya nyuklia ya JCPOA na kuiwekea Iran vikwazo vikubwa zaidi ambavyo havijawahi kutokea. Ijapokuwa awali serikali ya Trump ilidai kuwa inataka mapatano ya nyuklia ya JCPOA yaangaliwe upya ndio maana imejitoa kwenye makubaliano hayo, lakini hivi sasa inatangaza waziwazi lengo lake hasa la kujitoa kwenye mapatano hayo.
-
Sudan yaendelea kushinikizwa ianzishe uhusiano wa kawaida na utawala wa Israel
Oct 17, 2020 03:49Sudan inaendelea kushinikizwa ili ianzishe uhusiano wa kawaida wa kidiplomasia na utawala wa Kizayuni wa Israel. Marekani imetangaza bayana kuwa, sharti la Sudan kuondolewa katika orodha ya nchi ambazo zinaunga mkono ugaidi ni nchi hiyo kukubali kuanza kufanya mazungumzo yenye lengo la kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel.
-
Sisistizo la Russia la kushirikiana kijeshi na Iran baada ya kuondolewa vikwazo vya silaha
Oct 16, 2020 23:12Kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa vikwazo vya silaha vya Iran vinamalizika tarehe 18 mwezi huu wa Oktoba 2020 baada ya kumalizika muda wa miaka mitano wa vikwazo hivyo. Russia ikiwa mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama na moja kati ya nchi wanachama wa kundi la 4+1 imesisitiza kwamba itashirikiana kijeshi na Iran baada ya kumalizika vikwazo licha ya Marekani kufanya juhudi za kuongeza muda wa vikwazo hivyo.
-
Watu million 8 watumbukia katika umasikini Marekani kutokana na corona
Oct 16, 2020 10:14Mamilioni ya Wamarekani wametumnbukia katika umasikini kutokana na atharii mbaya za janga la corona kwa uchumi wa nchi hiyo.
-
Russia yasema Marekani ndio mkiukaji mkubwa zaidi wa haki za binadamu duniani
Oct 16, 2020 03:11Marekani ambayo ni mkiukaji mkubwa zaidi wa haki za binadamu duniani na ambayo ina rekodi nyeusi kuhusu suala hilo, daima imekuwa ikikwepa kujibu maswali ya raia wake kuhusu jambo hilo na badala yake kuzituhumu nchi nyingine ikiwemo Russia kwamba haziheshimu haki za binadamu.
-
Sera za upande mmoja za Marekani ni tishio kwa jamii ya kimataifa
Oct 15, 2020 23:05Mjumbe wa Iran katika Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa amesema kuendelea sera za kujichukulia maamuzi ya upande mmoja ni tishio la kimataifa katika kuunga mkono na kuinua kiwango cha haki za binadamu.