-
Marekani kuzuia pesa za mafuta za Baghdad wanajeshi wake wakitimuliwa Iraq
Jan 12, 2020 21:08Utawala wa Washington umetishia kuzuia akaunti za benki zenye mabilioni ya dola za Iraq, iwapo serikali ya Baghdad itakeleza mpango wake wa kuwatimua nchini humo wanajeshi wa Marekani.
-
Akthari ya Wamarekani hawaungi mkono namna Trump anavyoamiliana na Iran
Jan 12, 2020 21:07Utafiti mpya wa maoni uliofanywa na shirika la Ipsos likishirikiana na kanali ya televisheni ya ABC News ya Marekani unaonyesha kuwa, aghalabu ya wananchi wa Marekani hawaungi mkono sera ghalati za Rais Donald Trump dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Hizbullah yasisitiza kuondoka wanajeshi wa Marekani eneo la Asia Magharibi
Jan 12, 2020 08:46Mwenyekiti wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza kuhusu kuondoka wanajeshi wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi kama jibu la kweli la mauaji ya kigaidi ya mashahidi Haj Qassem Soleimani na Abu Mahdi al Muhandis.
-
Mwakilishi wa Iran UN: Marekani iondoke magharibi mwa Asia
Jan 11, 2020 23:08Balozi na mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Luteni Jenerali shahidi Qassem Soleimani ni shujaa wa mapambano dhidi ya ugaidi katika eneo la magharibi mwa Asia na kuongeza kuwa, Marekani inapaswa kuondoka katika eneo hilo.
-
Russia: Hatua za Marekani zimesababisha maafa ya ndege ya Ukraine mjini Tehran
Jan 11, 2020 23:07Naibu Mkuu wa Kamisheni ya Usalama wa Taifa na Ulinzi ya Bunge la Russia (Duma) amesema kuwa, ni muhimu kutilia maanani uhakika kwamba, hatua za kichochezi za Marekani dhidi ya Iran ndiyo sababu ya tukio chungu la kuangushwa ndege ya Ukraine mjini Tehran.
-
Venezuela yaionya Marekani na kuitaka iache kuingilia masuala yake ya ndani
Jan 11, 2020 09:03Serikali ya Venezuela imeionya Marekani na kuitaka iache mchezo wake wa kuingilia masuala ya ndani ya Caracas.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran; muendelezo wa sera za mashinikizo ya juu kabisa
Jan 11, 2020 04:43Katika zama za utawala wa Rais Donald Trump, serikali ya Marekani imekuwa ikifuatilia sera za mashinikizo ya juu kabisa dhidi ya Iran na katika fremu hiyo mnamo Mei 8 2018, Washington ilitangaza kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na baada ya hapo ikaweka vikwazo shadidi zaidi dhidi ya Iran. Pamoja na kuwa vikwazo hivyo havijafikia malengo yaliyokusudiwa, Marekani inasisitiza kuendeleza sera yake ya kushadidisha vikwazo.
-
Amir Hatami: Marekani inapaswa kuhitimisha haraka uvamizi wake Asia Magharibi
Jan 11, 2020 01:20Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, ili kukabiliana na mizozo na uzushaji wa migogoro na ukosefu wa amani katika eneo la Asia Magharibi, kuna ulazima wa uvamizi na uangiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya eneo hili kuhitimishwa haraka iwezekanavyo.
-
Mashauriano ya kidiplomasia ya Iran kwa ajili ya kuarifisha jinai za Marekani
Jan 10, 2020 07:30Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na viongozi wa nchi kadhaa jirani, nchi za Ulaya na Afrika kwamba Iran inaunga mkono amani na usalama lakini haitakaa kimya mbele ya vitimbi vya Marekani.
-
Umati mkubwa wa Wairaqi wakusanyika mahali walipouawa shahidi Qassem Soleimani na Abu Mahdi al-Muhandis
Jan 10, 2020 04:41Mamia ya Wairaqi wamekusanyika mahali makombora ya jeshi la kigaidi la Marekani yalipoulenga msafara wa magari yaliyokuwa yamewabeba Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu na Abu Mahdi al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Jeshi la Kujitolea la Wananchi wa Iraq la Al-hashdu-Sha'abi na kulaani jinai hiyo ya Marekani.