-
Kuwait: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haipasi kuwa chini ya vikwazo
Dec 13, 2019 23:36Mwakilishi wa Kuwait katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haipasi kuwa chini ya vikwazo.
-
Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini Marekani chaongezeka maradufu
Dec 13, 2019 23:34Wizara ya Kazi nchini Marekani imetoa ripoti mpya ikisema kuwa kiwango cha ukosefu wa ajira nchini humo kimeongezeka kwa kiwango cha juu.
-
Syria yakosoa jinai zinazofanywa na Marekani dhidi ya binadamu na haki zake
Dec 13, 2019 06:59Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria imeikosoa Marekani kutokana na jinai zake dhidi ya ubinadamu na haki za binadamu katika maeneo mbalimbali ya dunia na imetoa wito wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusiana na jinai hizo.
-
Guterres asisitiza kuwa vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran vinakiuka azimio 2231
Dec 13, 2019 05:33Rais Donald Trump wa Marekani ni mpinazni mkali wa mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) akiyataja kuwa ni mapatano mabaya zaidi kuwahi kufikiwa katika historia ya Marekani.
-
Ripoti: Watoto walioko katika jela nchini Marekani wanabakwa na kudhalilishwa
Dec 12, 2019 21:13Ripoti mpya ya Taasisi ya Takwimu za Sheria ya Marekani imefichua kuwa, asilimia 7.1 ya watoto walioko katika mamia ya jela na vituo vya kurekebisha tabia vya watoto nchini Marekani walibakwa na kufanyiwa vitendo vingine vya udhalilishaji katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.
-
Mpango wa Pentagon wa kuongeza idadi ya askari wa Marekani barani Ulaya kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa
Dec 11, 2019 04:41Donald Trump, rais machachari na mwenye makeke wa Marekani amewahi kusikika mara kadhaa akiwalaumu na kuwakosoa waitifaki wa Washington wa barani Ulaya na hata kutishia kwamba, nchi yake haitakuwa tayari kuendelea kugharimika kwa ajili ya usalama wa nchi za bara hilo; hata hivyo mpango uliotangazwa na Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon wa kuongeza idadi ya askari wa nchi hiyo barani Ulaya umeyatoa maanani madai hayo ya Trump.
-
Luxembourg yaiandikia barua EU kuhusu kutambuliwa rasmi taifa la Palestina
Dec 09, 2019 23:50Luxembourg imeuandikia barua Umoja wa Ulaya, ikiutaka umoja huo uitambue rasmi nchi huru ya Palestina.
-
Hafla ya "Milango Wazi" yafanyika katika misikiti Marekani kwa ajili ya kuutangaza Uislamu
Dec 09, 2019 08:53Waislamu katika jimbo la Ohio nchini Marekani wamefanya hafla iliyopewa jina la "Milango Wazi" katika misikiti yao kwa kuwakaribisha wasio Waislamu misikitini humo ili waweze kuuelewa Uislamu.
-
Seneta wa Republican: Saudi Arabia ni mhusika wa ugaidi dhidi ya Marekani
Dec 09, 2019 04:33Seneta wa chama tawala cha Republican nchini Marekani amesema Saudi Arabia inabeba dhima ya matukio ya kigaidi dhidi ya Marekani.
-
Azimio la Kongresi ya Marekani dhidi ya uvamizi wa utawala wa Kizayuni katika eneo la Ukingo wa Magharibi
Dec 08, 2019 23:11Serikali ya rais Donald Trump imekuwa ikitekeleza hatua zisizo za kawaida katika uwanja wa kuunga mkono vitendo vilivyo kinyume cha sheria vya utawala haramu wa Israel dhidi ya taifa la Palestina.