-
Afisa wa zamani wa CIA: Mauaji ya Haniyeh yamefanyika kwa msaada wa Marekani na Uingereza
Aug 03, 2024 00:58Larry C. Johnson, afisa mstaafu wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), amesema kuwa mauaji yalioyofanywa na Israel dhidi ya Ismail Haniyeh, mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Hamas, yamevuka mstari mwekundu na kuongeza kuwa mauaji hayo yametekelezwa kwa taarifa na msaada wa Uingereza na Marekani.
-
Tovuti ya Uingereza: Utawala wa Marekani ni kipofu kiasi kwamba unamhami mtu kama Netanyahu
Jul 29, 2024 22:59"Kuporomoka kwa dola kunakuwa jambo lisiloepukika mara tu watawala wake wanapopoteza kabisa hisia za jinsi walivyokuwa wapuuzi na wa kutisha", hivi ndivyo ilivyoandika tovuti ya Uingereza ya Middle East Eye ikizungumzia fedheha kubwa ya Congress ya Marekani ya kumkaribisha na kumpigia makofi nduli na Adolf Hitler wa zama hizi, Benjamin Netanyahu, anayeendelea kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Marekani yahamisha silaha zilizopigwa marufuku kutoka Ujerumani kwenda Ukraine
Jul 28, 2024 04:34Vyombo vya habari vya Ujerumani vimefichua kuwa nchi hii inahifadhi mabomu yaliyopigwa marufuku ya vishada ya Marekani na kwamba inapanga kuyahamishia Ukraine.
-
Kikao cha Baraza la Usalama kuhusu vita vya Gaza; muendelezo wa uungaji mkono wa Marekani kwa utawala wa Kizayuni
Jul 27, 2024 22:59Suala la hali mbaya ya Ukanda wa Gaza siku ta Ijumaa kwa mara nyingine tena liliwekwa katika ajenda ya utendaji ya kikao cha nchi 15 wanachama wa Baraza la Usalama la UN sambamba na Bejamin Netanyahu Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni kushiriki katika kikao hicho huko Marekani.
-
Marekani na UK zafanya mashambulizi ya anga katika mji wa Hudaydah huko Yemen
Jul 27, 2024 03:43Marekani na Uingereza zimefanya mashambulia ya anga dhidi ya Bandari ya al Hudaydah iliyoko magharibi mwa Yemen.
-
HAMAS: Kauli ya Marekani ni uongo mtupu, Wapalestina Ghaza wanauawa kwa silaha zake
Jul 26, 2024 09:29Mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "Madai ya Washington kwamba inatiwa wasiwasi na hali ya kibinadamu na inasikitishwa na machungu na mateso wanayopata watu wa Ghaza ni uongo wa Kimarekani".
-
Amnesty International: Marekani mshirika wa Israel katika mauaji ya kimbari Palestina
Jul 25, 2024 03:41Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International imeonya Marekani kuhusu kuupa silaha utawala wa Kizayuni katika vita vya Gaza na kutangaza kuwa, Washington ni mshirika wa utawala huo katika mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
-
Duru mpya ya mazungumzo ya pamoja ya usalama kati ya Marekani na Iraq mjini Washington
Jul 24, 2024 07:44Alina Romanowski, balozi wa Marekani mjini Baghdad, alitangaza siku ya Jumatatu kuhusu kuanza mazungumzo kati ya Marekani na Iraq huko Washington mji mkuu wa Marekani ajenda kuu ikiwa ni "mustakabali wa muungano wa kimataifa."
-
Biden ajitoa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais wa Marekani
Jul 22, 2024 22:53Hatimaye, Joe Biden, Rais wa Kidemokrati wa Marekani mwenye umri wa miaka 81, amejiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kuwania urais wa nchi hiyo baada ya mijadala mingi kuhusu kugombea kwake katika uchaguzi wa Novemba 5 mwaka huu, na kumuunga mkono Kamala Harris, makamu wake kama mgombea wa kiti hicho.
-
Republican: Biden ni punguani, asiachiwe kitufe cha silaha za nyuklia
Jul 22, 2024 07:27Muda mfupi baada ya Rais Joe Biden wa Marekani kutangaza kujiondoa katika kinyang'anyiro cha kutetea kiti chake cha urais, viongozi waandamizi wa chama cha Republican wamesema mwanasiasa huyo mwenye miaka 81 hapasi kuachiwa nywila (kodi) za kitufe cha silaha za nyuklia kutokana na matatizo ya kisaikolojia yanayomsumbua.