-
UN yatakiwa kuitisha mkutano wa dharura kufuatia mauaji ya kikatili ya Floyd Marekani
Jun 09, 2020 03:30Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limetakiwa kuitisha mkutano wa dharura wa kujadili mauaji ya kikatili yaliyofanywa na polisi mzungu dhidi ya raia mwenye asili ya Afrika, George Floyd mwishoni mwa mwezi uliopita wa Mei.
-
Wanamgambo wa CODECO waua watu 16 Kongo DR
Jun 04, 2020 03:06Watu wasiopungua 16 wameuawa katika shambulizi jingine la kutisha la wanamgambo wa CODECO huko kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Gambia yataka uchunguzi wa mauaji ya mtoto wa mwanadiplomasia nchini Marekani
Jun 04, 2020 00:16Serikali ya Gambia imeitaka Marekani ianzishe uchunguzi mara moja wa mauaji ya mtoto wa kiume wa mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa nchi hiyo ya Kiafrika katika jiji la Atlanta, jimboni Georgia.
-
Genge la wabeba silaha laua 18 Nigeria, laiba maelfu ya mifugo
Jun 01, 2020 05:52Genge la watu waliojizatiti kwa silaha limeshambulia kijiji kimoja huko kaskazini magharibi mwa Nigeria na kuua watu 18 mbali na kuiba maelfu ya mifugo ya wakazi wa kijiji hicho.
-
AU yalaani ukatili wa polisi ya Marekani dhidi ya raia weusi
May 30, 2020 03:44Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amelaani vikali mauaji ya raia mweusi nchini Marekani katika jimbo la Minnesota, licha ya kuwa hakuwa na silaha yoyote.
-
Watu wengine 40 wauawa kwa kukatwa mapanga Kongo DR
May 28, 2020 03:29Watu wasiopungua 40 wameuawa katika shambulizi jingine la kutisha la wanamgambo wa ADF huko kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, mpakani na Uganda.
-
Amnesty: Marekani imepunguza idadi ya raia iliyowaua katika operesheni za kijeshi
May 07, 2020 03:16Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limetofautiana na idadi iliyotangazwa na Washington ya raia waliouawa katika operesheni za kijeshi za Marekani mwaka jana 2019 katika nchi mbali mbali duniani.
-
Magaidi 129 wameuawa ndani ya mwezi mmoja na maafisa usalama Msumbiji
Apr 29, 2020 06:42Waziri wa Mambo ya Ndani wa Msumbiji ametangaza habari ya kuuawa makumi ya wanachama wa magenge ya kigaidi kaskazini mwa nchi katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.
-
UN yalaani mauaji ya wasichana na wanawake mjini Tripoli, Libya
Mar 20, 2020 08:36Umoja wa Mataifa umelaani shambulizi la mabomu katika mji mkuu wa Libya Tripoli, ambalo liliua na kujeruhi watoto wa kike na wanawake kadhaa.
-
Mwaka mmoja baada ya mauaji ya Waislamu New Zealand, usiri unatawala uchunguzi kuhusu mauaji hayo
Mar 14, 2020 22:58Ripoti iliyotayarishwa na gazeti la Washington Post inasema kuwa, uchunguzi wa serikali ya New Zealand wa kutaka kupata majibu yanayoweka wazi jinsi mhalifu aliyefanya mauaji ya kutisha ya Waislamu 51 waliokuwa wakitekeleza ibada misikitini, alivyoweza kufanya mauaji hayo, unaendelea kwa usiri mkubwa, jambo ambalo limezusha wasiwasi wa wachambuzi wa mambo ya jamii ya Waislamu wa New Zealand.