-
Israel yaandaa muswada wa 'kifashisti' wa kuruhusu utoaji wa hukumu ya adhabu ya kifo kwa Wapalestina
Nov 03, 2025 22:55Kamati moja ya wabunge wa utawala wa kizayuni wa Israel imeidhinisha muswada wa kuanzisha utoaji wa adhabu ya kifo kwa Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala huo, na kufungua njia ya kusomwa hoja hiyo kwa mara ya kwanza bungeni licha ya kuandamwa na lawama nyingi.
-
Israel yaendelea kuwatesa kwa njaa Wapalestina kwa kuruhusu 24% tu ya misaada kuingizwa Ghaza
Nov 02, 2025 03:20Mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimetangaza kuwa utawala wa kizayuni wa Israel umeruhusu kuingizwa katika eneo hilo sehemu ndogo tu ya misaada ya kibinadamu kinyume na ilivyoafikiwa katika makubaliano ya usitishaji mapigano yanayosimamiwa na serikali ya Marekani, ambayo yalianza kutekelezwa mwezi uliopita.
-
UNICEF: Usitishaji vita Gaza ni fursa muhimu ya kukidhi mahitaji ya watoto
Oct 27, 2025 23:44Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaweza kuwa "fursa muhimu" ya kulinda maisha, utu na mahitaji muhimu ya watoto milioni moja wa Kipalestina.
-
Hamas yasisitiza haki ya Wapalestina ya kuwa na nchi huru; yasema imesitisha mapigano Gaza
Oct 27, 2025 02:58Afisa wa ngazi ya juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesisitiza dhamira isiyoyumba ya harakati hiyo ya kutekeleza usitishaji vita huko Gaza na kusema Wapalestina hawataki kitu chochote isipokuwa haki yao inayotambulika kimataifa ya kuwa na nchi huru.
-
MSF: Israel inaendelea kutumia misaada ya Gaza kama silaha ya vita
Oct 26, 2025 23:13Afisa mkuu wa shirika la kimataifa la misaada ya kibinadamu la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) anasema utawala wa Israel unaendelea kutumia misaada ya kibinadamu huko Gaza kama silaha ya vita dhidi ya Wapalestina.
-
Kwa nini UNRWA huko Gaza inalengwa kwa mashinikizo ya kisiasa?
Oct 26, 2025 02:39Mkuu wa Shirika la Misaada na Ajira kwa Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amesema: Vita vya Gaza vimeonyesha kwamba sheria za kimataifa hazizingatiwi kabisa.
-
Ripoti: Asilimia 97 ya shule za Gaza zimeharibiwa kwa mashambulizi ya Israel
Oct 19, 2025 23:58Ripoti rasmi zinasema, mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel yameharibu asilimia 97 ya shule za Ukanda wa Gaza na hivyo kuhatarisha mustakbali wa kielimu wa wanafunzi laki tatu wa Kipalestina katika eneo hilo.
-
HAMAS: Hatutajifunga kukabidhi silaha mpaka yatakapofanyika mazungumzo zaidi
Oct 18, 2025 23:12Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa haitajifunga moja kwa moja kukabidhi silaha na inatumai usitishaji vita na utawala wa kizayuni wa Israel utadumu kwa muda wa miaka mitatu hadi mitano ili kuijenga upya Ghaza.
-
Wananchi wa Uruguay waandamana wakitaka kukatwa uhusiano na Israel
Oct 11, 2025 05:55Maelfu ya wananchi wa Uruguay waliingia mitaani na mabarabarani jana Ijumaa, kushiriki maandamano ya kuitaka serikali yao itambue mzozo wa kibinadamu unaoendelea Gaza kama mauaji ya halaiki, sanjari na kukata uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi na Israel.
-
Makundi ya Muqawama ya Palestina yakataa Ghaza kuwa chini ya utawala na usimamizi wa wageni
Oct 10, 2025 23:52Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina, HAMAS pamoja na makundi mengine washirika ya Muqawama wa Palestina yamesisitiza kuwa uamuzi wowote kuhusu utawala wa baadaye wa Ghaza ni "suala la ndani la Palestina" na kupinga vikali eneo hilo kutawaliwa na kusimamiwa na maajinabi.