-
Newsweek: Wanajeshi 270 wa Marekani wameuawa katika mashambulio ya SEPAH
Jan 10, 2020 00:34Kwa mara ya kwanza toleo la mtandao la gazeti la kila wiki la Newsweek la Marekani limefichua kwamba, kwa uchache wanajeshi 270 wa nchi hiyo wameangamizwa katika shambulio la usiku wa kuamkia Jumatano lililofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH katika kambi mbili za Marekani za Ain al Asad na Erbil nchini Iraq.
-
Majibu ya kutapatapa ya Trump baada ya Iran kupiga kwa makombora kambi za Marekani + Video
Jan 09, 2020 10:50Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetekeleza kivitendo ahadi yake ya kutoa jibu kali kwa jinai ya Marekani ya kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH.
-
Kiongozi Muadhamu: Tumempiga kibao tu adui, anachopaswa kufanya Marekani ni kuondoka eneo hili
Jan 08, 2020 13:09Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mashambulio ya makombora yaliyofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH katika kambi mbili za Marekani nchini Iraq ni kibao cha uso tu alichopigwa adui huyo.
-
Rouhani: Majibu kamili ya Iran ni kukatwa miguu ya Wamarekani Asia Magharibi
Jan 08, 2020 11:33Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amegusia majibu makali yaliyotolewa usiku wa kuamkia leo na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH ya kuwashambulia magaidi wa Kimarekani katika kambi zao mbili za kijeshi nchini Iraq na kusema kuwa, majibu kamili ya Iran kwa jinai za Wamarekani ni kukatwa miguu yao kwenye eneo hili.
-
Jibu kali la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa jinai na ugaidi wa vikosi vamizi vya Marekani
Jan 08, 2020 08:14Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, IRGC, mapema leo Jumatano alfajiri, katika kujibu jinai na ugaidi wa wanajeshi vamizi wa Marekani ambao walimuua shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, limevurumisha makombora ambayo yamelenga kituo cha anga cha jeshi vamizi na la kigaidi la Marekani cha Ain al-Assad nchini Iraq.
-
Vitisho vya Trump vya kuiwekea vikwazo Iraq, kushindwa kwingine kwa Washington
Jan 07, 2020 07:44Jinai kubwa ya Marekani ya kumuua kigaidi Meja Jenerali Qassem Soleimani na Abu Mahdi Al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Harakati ya Kujitolea ya Wananchi wa Iraq ya Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq, imeibua radiamali kali ya bunge la nchi hiyo ya Kiarabu na kuipelekea kupitisha sheria ya kuvitimua vikosi vya muungano vamizi wa eti kupambana na Daesh (ISIS) unaojumuisha askari wa Marekani.
-
Netanyahu apatwa na kiwewe cha jibu kali la muuqawama kufuatia jinai dhidi ya Luteni Soleimani
Jan 07, 2020 05:00Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa Utawala Haramu wa Kizayuni wa Israel, amelegeza msimamo kunako msimamo wake wa awali wa kuunga mkono jinai ya kigaidi iliyofanywa na Marekani ya kuwaua shahidi viongozi wa mrengo wa muqawama, ambapo sasa amesema kuwa Israel haikuhusika katika shambulizi hilo la Marekani katika uwanja wa ndege wa Baghdad, Iraq.
-
Rais Hassan Rouhani ajibu vitisho vya Trump asema: 'Kamwe usilitishe taifa kubwa la Iran'
Jan 07, 2020 04:52Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa radiamali yake kufuatia vitsiho vya Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu kuyalenga baadhi ya maeneo ya Iran kupitia ujumbe alioutuma kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter, ambapo amemuonya kwa kusema: "Kamwe usilitishe taifa kubwa la Iran."
-
Harakati ya Hizbullah ya Iraq yampa onyo kali Rais Donald Trump wa Marekani
Jan 07, 2020 04:41Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Iraq imemuonya Rais Donald Trump wa Marekani kwamba iwapo ataiwekea vikwazo nchi hiyo, basi harakati hiyo itazuia usafirishaji mafuta ya kwenda soko la nchi hiyo.
-
Zarif: Uwepo wa kishetani wa Marekani Asia Magharibi unaelekea kufika ukingoni
Jan 07, 2020 04:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria kujitokeza mamilioni ya Wairani katika mazishi ya mashahidi wa jinai ya hivi karibuni ya Marekani na kusema: "Uwepo wa kishetani wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi unaelekea kufika ukingoni."