-
Iran yalaani hatua ya Wazayuni wa Israel ya kuchoma moto Qur'ani Tukufu
Jun 24, 2023 10:07Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali kitendo cha walowezi wa Kizayuni cha kuvunjia heshima Qur'ani Tukufu wakati wa mashambulizi ya askari wa Israel dhidi ya misikiti katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Hekaya za Aya (1)
Jun 17, 2023 06:44Assalam Alaykum Warahmatullahi Wabarakatuh. Hamjambo na karibuni kuwa nasi katika sehemu ya kwanza ya kipindi chetu kipya tulichokipa jina la Hekaya za Aya ambacho kwa hakika kinazungumzia sababu, kisa au tukio lililopelekea kuteremshwa Aya mbalimbali za Qur'ani Tukufu.
-
Polisi ya Canada yamfungulia mashtaka ya uhalifu wa chuki aliyeshambulia msikiti, kuchana Qur'ani
Apr 10, 2023 07:55Polisi ya Canada imetangaza kuwa imemkamata na kumfungulia mashtaka mwanamume mmoja kwa kile kilichoelezwa kuwa ni "tukio la chuki" katika msikiti mmoja wa jimbo la Ontario Alhamisi iliyopita, baada ya kuhujumu Waislamu, kuwatishia na kuwatusi.
-
Qari wa Iran aibuka mshindi katika Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu Saudi Arabia
Apr 08, 2023 11:46Qari Yunes Shahmoradi kutoka Iran ameibuka mshindi katika toleo la pili la Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya Otr Elkalam nchini Saudi Arabia.
-
Wahindu wenye msimamo mkali washambulia shule ya Kiislamu na kuchoma nakala za Qur'ani na maelfu ya vitabu
Apr 04, 2023 13:30Wanaharakati kwenye majukwaa ya mawasiliano ya kijamiii ya India wamechapisha picha zinazoonyesha shule ya Kiislamu ikiteketea kwa moto katika jimbo la Bihar, baada ya kushambuliwa na Wahindu wenye msimamo mkali siku ya Ijumaa, na kusababisha uharibifu mkubwa.
-
Yemen yasusia bidhaa nchi za Ulaya zinazohusika na kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu
Apr 03, 2023 08:33Yemen imepiga marufuku kuingia nchini humo bidhaa zinazozalishwa na nchi za Ulaya ambazo zimewezesha kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu, ambapo kiongozi wa harakati ya muqawama ya Ansarullah ameitaja hatua hiyo kuwa ni "vikwazo vya kiuchumi".
-
Uturuki yawasilisha malamiko rasmi kuhusu kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu huko Denmark
Apr 02, 2023 03:06Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imemwita balozi wa Denmark nchini humo ili kutoa malalamiko yake ya kupinga kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu katika nchi hiyo ya Ulaya.
-
Ansarullah yalaani kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu
Mar 31, 2023 02:11Harakati ya Ansarullah ya Yemen imelaani vitendo vya kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu nchini Denmark na katika nchi nyingine za Ulaya.
-
Iran yalaani vitendo vya kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu Denmark
Mar 28, 2023 03:03Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani wimbi la kuvunjiwa heshima Qur'ani Tukufu na makundi yenye misimamo mikali ya mrengo wa kulia nchini Denmark na katika nchi nyingine za Ulaya.
-
Atakayemkabidhisha askari wa Ukraine aliyeivunjia heshima Qur'ani kuzawadiwa $168,000
Mar 19, 2023 12:33Rais Madan Kadyrov, wa eneo la Russia linalojiendeshea mambo yake la Chechnya ametenga zawadi ya ruble milioni 10 za Kirusi ambazo ni sawa na dola 168,000 za Kimarekani kwa atakayefanikisha kukamatwa akiwa hai, askari wa jeshi la Ukraine aliyeivunjia heshima Qur'ani tukufu kwa kuichoma moto nakala ya kitabu hicho kitakatifu.