-
Russia: Marekani na Uingereza zinaeneza machafuko ndani ya Syria kupitia magenge ya kigaidi
Nov 29, 2024 08:11Russia imesema madola makubwa ya Magharibi yanayoongozwa na Marekani yanaendelea na vitendo vyao vya chuki dhidi ya Syria kwa kuwaunga mkono wanamgambo wanaoipinga serikali ya Damascus pamoja na makundi ya kigaidi ya kitakfiri katika kila pembe ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Rais wa Russia asisitiza kuanzishwa mfumo wa dunia wa kambi kadhaa na wa haki zaidi
Nov 27, 2024 09:00Rais Vladimir Putin wa Russia amezungumza sambamba na kuwadia safari yake ya kuitembelea Kazakhstan na kusisitiza kuwa, nchi hizo mbili ziko mstari wa mbele katika mchakato wa kuunda mfumo wa dunia wa kambi kadhaa na wenye haki zaidi na pande hizo mbili zina misimamo inayofanana kuhusu mahusiano ya kimataifa na masuala ya usalama wa dunia.
-
Spika wa Uturuki: Kwa maamuzi ya Mahakama mbili za Kimataifa, Israel inaona mwisho wake unakaribia
Nov 27, 2024 08:36Spika wa Bunge la Uturuki Numan Kurtulmus amesema, hati ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) ya kukamatwa waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na waziri wa zamani wa ulinzi wa utawala huo Yoav Gallant ni kielelezo cha hatua nyingine kubwa inayoonyesha kuwa Israel sasa "inagusika".
-
Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya atoa indhari: Mustakabali wa EU uko 'hatarini'
Nov 26, 2024 03:12Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya anayemaliza muda wake Josep Borrell ametoa indhari kuwa mustakabali wa umoja huo uko hatarini kutokana na kukabiliwa na migogoro mingi kwa wakati mmoja, na akasisitiza kwamba EU haiwezi tena kuitegemea Marekani kwa ajili ya ulinzi wake.
-
Jumanne, 26 Novemba, 2024
Nov 25, 2024 22:54Leo ni Jumanne 24 Mfunguo Nane Jamadul-Awwal 1446 Hijria mwafaka na tarehe 26 Novemba 2024.
-
Russia yakosoa hatua ya Magharibi dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya IAEA
Nov 25, 2024 00:03Ubalozi wa Russia mjini Tehran umekosoa hatua ya nchi za Magharibi dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA).
-
Kuingia vita vya Ukraine katika hatua mpya na kuzidisha mzozo kati ya Russia na NATO
Nov 23, 2024 22:56Matukio ya hivi karibuni katika vita vya Ukraine, yaani uamuzi wa nchi za Magharibi wa kutoa ruhusa kwa Ukraine kuishambulia Russia kwa kutumia silaha za masafa marefu za Marekani na Ulaya kwa upande mmoja, na Russia kutumia w kombora jipya la masafa ya kati lenye kasi ya zaidi ya sauti dhidi ya Ukraine kama tahadhari kali kwa Magharibi, kumeibua mgogoro mkubwa na usio na kifani kati ya Russia na NATO.
-
Amri mpya ya Putin na kuongezeka uwezekano wa kutumiwa silaha za nyuklia
Nov 20, 2024 07:53Rais Vladimir Putin wa Russia Jumanne, Novemba 19, alitia saini amri ambayo inaipa Moscow ruhusa ya kutumia silaha za nyuklia dhidi ya "nchi isiyo na silaha za nyuklia" ilimradi nchi hiyo iwe inaungwa mkono na nguvu za nyuklia.
-
Siku 1000 za vita vya Ukraine na mustakabali wake usiojulikana
Nov 19, 2024 23:06Jumatatu ya juzi 18 Novemba, 2024, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilifanya mkutano mjini New York, kwa mnasaba wa siku elfu 1000 za Vita vya Ukraine.
-
Ombi la Antonio Guterres la kuzuia kuongezeka mivutano katika vita vya Ukraine
Nov 19, 2024 03:45Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kuzuia kuongezeka mapigano nchini Ukraine.