Feb 18, 2016 02:12
Tume ya uchaguzi nchini Uganda imewaonya vikali wenye nia ya kuvuruga zoezi la upigaji kura linalofanyika leo (Alkhamisi) na kusisitiza kuwa, watu wa aina hiyo watachukuliwa hatua kali za kisheria. Tume hiyo pia imesisitiza kuwa uchaguzi wa leo nchini Uganda utakuwa huru na wa haki.