-
Macron aendeleza vitendo vya kuuhujumu Uislamu; Trump aparamia mawimbi
Oct 30, 2020 23:08Kushtadi vitendo vya chuki na hujuma dhidi ya Uislamu nchini Ufaransa vinavyokwenda sambamba na uungaji mkono wa Rais wa nchi hiyo Emmanuel Macron kwa kisingizio kutetea uhuru wa kusema na kujieleza kumekabiliwa na radiamali mbalimbali na kuifanya nchi hiyo kubwa ya Ulaya ikabiiwe na wimbi kubwa la hasira.
-
Jumuiya Maulamaa wa Palestina: Nchi za Kiislamu zivunje uhusiano wa kidiplomasia na Ufaransa
Oct 30, 2020 13:16Jumuiya ya Maulamaa na Wanatablighi wa Palestina imelaani matamshi ya kifidhuli aliyotoa rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ya kuunga mkono kitendo cha jarida la nchi hiyo la Charlie Hebdo cha kumvunjia heshima Bwana Mtume Muhammad SAW na kuzitolea mwito nchi za Kiislamu wa kuvunja uhusiano wa kidiplomasia na Ufaransa.
-
Waziri Mkuu wa Canada apingana na Macron, asema Uislamu hauna mfungamano na ugaidi
Oct 30, 2020 05:24Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau amesema kuwa gaidi aliyetekeleza hujuma ya kigaidi katika mji wa Nice nchini Ufaransa hawakilishi dini ya Uislamu wala Waislamu, na kwamba watu wote wanapasa kukiri ukweli huo.
-
Waislamu wa Ufaransa walaani shambulio la kigaidi lililotokea nchini humo
Oct 29, 2020 23:01Baraza la Waislamu wa Ufaransa limelaani shambulio la kigaidi lililotokea nchini humo.
-
Katibu Mkuu wa Ansarullah: Macron ni kikaragosi kinachochezeshwa na Wazayuni
Oct 29, 2020 23:01Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema rais Emmanuel Macron wa Ufaranmsa ni kikaragosi kinachochezeshwa na Wazayuni kichukue hatua za kuutusi na kuuvunjia heshima Uislamu.
-
Ujumbe wa Kiongozi Muadhamu kwa vijana wa Ufaransa, awataka wamhoji Macron kwa nini anamtusi Mtume wa Mungu kwa jina la uhuru wa maoni?
Oct 29, 2020 07:52Kingozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amewatumia ujumbe vijana wa Ufaransa akiwataka wamhoji Rais wa nchi hiyo, Emmanuel Macron kwa nini kwa nini anamtusi Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa jina la uhuru wa maoni?
-
Kiongozi Muadhamu aushangaa undumakuwili wa Rais Macron wa Ufaransa
Oct 29, 2020 03:57Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameeleza kushangazwa kwake na undumakuwili wa Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa kwa kulikingia kifua jarida la Charlie Hebdo la nchini hiyo ya Ulaya kwa kuchapisha tena vibonzo vya kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW, kwa kisingizio cha uhuru wa kujieleza.
-
Maandamano ya kulaani misimamo ya Macron dhidi ya Uislamu yafanyika Iran na Iraq
Oct 29, 2020 03:23Maelfu ya Waislamu katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Iraq wamefanya maandamano ya kulaani hatua ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ya kuunga mkono vitendo vya kuvunjiwa heshima Mtume Muhammad SAW na matukufu ya Kiislamu.
-
EuroMed Rights yakosoa chuki na uhasama Wa viongozi wa Ufaransa dhidi ya Waislamu
Oct 28, 2020 23:25Kituo cha Haki za Binadamu Ulaya na Mediterania (EuroMed Rights) kimeItaja hatua ya viongozi wa Ufaransa ya kueneza chuki na uhasama dhidi ya Waislamu kuwa ni hatari kubwa.
-
Ayatullah Larijani ataka Waislamu waungane kukabili chuki dhidi yao
Oct 28, 2020 04:22Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Iran amelaani vikali hatua ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ya kuunga mkono kitendo cha kifidhuli cha jarida la Charlie Hebdo cha kuchapisha tena vibonzo vya kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW na kusisitiza kuwa, kuna udharura wa Waislamu kuwa na umoja na ushirikiano katika kukabiliana na chuki dhidi yao na Uislamu.