-
UN yatahadharishwa: Tafsiri ya 'chuki dhidi ya Uyahudi' isitumiwe kudhibiti ukosoaji dhidi ya unyama wa Israel
Apr 22, 2023 08:36Zaidi ya mashirika 100 ya kutetea haki za binadamu na haki za kiraia yameuonya Umoja wa Mataifa dhidi ya matumizi ya tafsiri ya chuki dhidi ya Wayahudi ambayo inaweza kutumiwa kuzuia ukosoaji wa uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu unaofanywa na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel na kudhoofisha uungaji mkono wa haki za Wapalestina.
-
Umoja wa Mataifa kujadili na kuamua kuhusu uhalali wa utawala wa Taliban
Apr 19, 2023 02:24Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa: taasisi hiyo itachunguza upya suala la uhalali wa serikali ya Taliban nchini Afghanistan ndani ya kipindi cha wiki mbili zijazo.
-
Dola bilioni 2.6 zinahitajika mwaka huu kusaidia Wasomali zaidi ya milioni saba wenye hali mbaya
Apr 06, 2023 03:54Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa dola bilioni 2.6 zinahitajika kwa ajili ya kuwasaidia mamilioni ya watu nchini Somalia ambako changamoto za mabadiliko ya tabianchi na mgogoro wa muda mrefu vimesababisha nchi hiyo kuwa na moja ya janga kubwa zaidi la kibinadamu duniani.
-
UN yaituhumu EU kuunga mkono jinai dhidi ya binadamu Libya
Mar 28, 2023 03:55Jopo la uchunguzi la Umoja wa Mataifa limesema kwamba, kuna ushahidi unaoonyesha kuwa jinai dhidi ya binadamu zimefanywa dhidi wa wananchi wa Libya na wahajiri waliokwama katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika, wakiwemo wanawake wanaolazimishwa kuingia kwenye utumwa wa kingono.
-
Indhari ya UN: Watu bilioni 2.4 hawatakuwa na maji mijini ifikapo mwaka 2050
Mar 22, 2023 23:23Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuchukuliwa hatua madhubuti sasa hivi kuhakikisha rasilimali adhimu ya maji inalindwa, kudhibitiwa ipasavyo na kupatikana kwa kila mtu.
-
UN, nchi za Kiarabu zalaani uropokaji wa Waziri wa Fedha wa Israel
Mar 21, 2023 22:49Umoja wa Mataifa na ulimwengu wa Kiarabu umelaani matamshi ya kichochezi yaliyotolewa hivi karibuni na Waziri wa Fedha wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Palestina.
-
Umoja wa Mataifa watahadharisha kuhusu ongezeko la joto duniani
Mar 21, 2023 07:01Umoja wa Mataifa umetangaza katika ripoti yake mpya kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa kwamba kuongezeka kwa joto la sayari ya dunia kumewaweka binadamu katika hatari ya kutoweka.
-
Kukosoa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kampeni za chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu
Mar 12, 2023 08:42Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amekosoa uenezaji hofu juu ya Uislamu na chuki za aina mbalimbali dhidi ya Uislamu na Waislamu duniani.
-
Guterres: Usawa wa jinsia duniani umesalia nyuma kwa miaka 300
Mar 07, 2023 03:46Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema dunia haijachukua hatua za maana kulinda haki za wanawake, na kwamba usawa wa jinsia katika kona zote za dunia inaonekana ajenda ambayo ipo karne nyingi nyuma kufikiwa.
-
Umoja wa Mataifa waanzisha uchunguzi katika mauaji ya watu wa asili wa Kanada
Mar 03, 2023 05:25Kufichuliwa mauaji ya wakazi asilia wa Kanada, hasa watoto, kumeibua kashfa kubwa dhidi ya nchi hiyo inayodai kuwa mtetezi wa haki za binadamu ulimwenguni. Kuhusiana na hilo, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuanza shughuli yake ya uchunguzi kuhusu mauaji hayo ya kimbari ya watu asilia wa Kanada.